JINA LA QURAAN: Zanjabil

 

MAJINA YA KAWAIDA: Ginger(Eng), Hinna,Hinnan (Arab), Zanjbil,Janzbil, ……….(Heb),Sonth,Adrak (Hindi), Tangawizi(kiswahili)

JINA LA KITAALAMU: Zingiber officinate

JAMII: Zingiberaceae

WAPI KATIKA QURAAN IMETAJWA:

76:17

Mwenyezi Mungu anasema:

"Na humo watanyweshwa kinywaji kilichochanganywa na Tangawizi."

(76:16)

Kinywaji cha pombe ambacho huko peponi watakinywa wale ambao hawajapata kunywa hapa duniani. Inaelezwa katika aya ya (Sura Dahr) kuwa kinywaji hicho kitachanganywa na Tangawizi.

 Tangawizi hapa inaelezwa kwa kuwa huko Arabuni zamani tangawizi ilikuwa inahusishwa sana na Wa-Arabu, kwa hivyo ndio mana imetajwa.

Kitarekh Tangawizi inaelezwa kuwa ni kipando cha nchi za India, lakini Zanzibar nayo kuna wakati ilikuwa ikipatikana kwa wingi, na hivi sasa Tangawizi yote itumiwao Zanzibar inatoka nje ya nchi, sijui wataalamu wakilimo wanaweza kutueleza nini?

Mtangawizi unaota chini ya ardhi na Tangawizi imekuwa inatumiwa kila mwahali duniani. Inavitu kama "Zingiberine, cineol, na borneol".

Mafuta ya Tangawizi, Ginger oleoresin na tangawizi kavu ni biashara kubwa duniani kote.

Tangawizi hutumika kuhifadhia vitu, hutumika katika vinywaji, biskuti, viungo vya mchuzi, mkate, beer, na hata shira mbali mbali hutengenezwa na mchanganyo wa tangawizi..

Mwenye kukosa utashi wa kula (loss of appetite) mchanganyiko wa tangawizi, sharbati ya ndimu na mchanganyo wa chumvi ya mawe huwa kinywaji kitachoweza kurejesha hamu na nguvu ya kula.

Inaaminika kwa wale wagonjwa wa kisukari kinywaji cha tangawizi husaidia kwa mgonjwa lakini kinywaji hicho kiwe bila ya kuchanganya na sukari.

Kusumbuliwa na kumwa na ufizi na kichwa (neuralgic headaches) mchanganyiko wa tangawizi kavu na maji huwa msaada mkubwa.

Ibn Sina ameelezea kwa mapana faida za tangawizi.

Nchi nyingi duniani husafirisha tangawizi zikiwemo India, Malaysia, Nigeria. Nchi ya India huingiza mapato ya wastani kwa kusafirisha Tangawizi katika nchi za Iran, Kuwait, Morocco, saud Arabia, Yemen, U.A.E, Uiengereza na hata Merekani.

Tangawizi itumiwao kwa kuhifadhi vyakula huzalishwa kwa wingi na nchi ya Hong Kong, Australia na China na kusafirishwa kwa wingi kwa nchi za Magaribi.

 

HADITHI

Anaeleza Abu Said Al Khudri kuwa;

“Mtawala wa Rumi (Rome) alituma kikapu cha Tangawizi kama ni zawadi kwa Bwana Mtume Muhammad SAW, na Bwana Mtume alimpa kipande kila mmoja katika Masahaba nami nikapata changu."

Abu Nu’im