AMALI (Matendo)
NI AINA NYINGI.
MOYO MSAFI NI
MOYO WA MWENYE KUAMINI.
KUUPENDA
UKWELI NA KUUFUNGULIA MOYO UISLAMU.
KUITIKIA MWITO
WA IMANI NA KUPENDA KUIONGEZA.
KULAINISHA
NYOYO KWA KUMDHUKURU MWENYEZIMUNGU.
DALILI ZA
KIELIMU ZINAZOITHIBITISHA IMANI JUU YA MWENYEZIMUNGU
UKIICHUNGUZA
BIDHAA ITAKUJULISHA BAADHI YA SIFA ZA MTENGENEZAJI
ALIYE HAI -
AMBAYE YUPO MILELE - (AL HAY)
MWENYE KUJUWA
(Kila kitu) - (AL ALIYM)
MWENYE UJUZI
WA KILA JAMBO - (AL KHABIYR)
MTOAJI WA
RIZIKI - (AL RAZZAAQ)
MMOJA TU ALIYE
PEKEE (AL WAAHIDUL AHAD)
MSINGI WA TATU
- ASIYEKUWA NA KITU HAWEZI KUTOA
MAMBO
YANAYOBABAISHA WATU NA MAJIBU YAKE.
ANAYEMJIBU
ALIYEDHIKIKA ANAPOMUOMBA
MSIMAMO WA
MAKAFIRI DHIDI DALILI ZA IMANI.
UZUSHI WA
MAMBO YANAYOBABAISHA
KUMJUA
MWENYEZIMUGU KWA MAJINA YAKE NA SIFA ZAKE
WAHYI NDIYO
NJIA BORA KATIKA KUYAJUA MAJINA NA SIFA ZA MWENYEZIMUNGU
KUMTAKASA
MWENYEZIMUNGU KWA KUTOMFANANISHA NA VIUMBE
KUYAAMINI
MAJINA NA SIFA ZA MWENYEZI MUNGU KAMA YALIVYO
HAIWEZEKANI
KUUJUWA MFANO WAKE
USHAHIDI
KWAMBA MUHAMMAD(SAW) NI MTUME WA MWENYEZIMUNGU
UFASAHA WA
QURANI NA KUTOKUCHOSHA KWAKE
QURANI YAELEZA
MAMBO YA GHAIBU
MIUJIZA YA
SAYANSI KATIKA QURANI
Nashuhudia kuwa hapana Mola anayestahiki kuabudiwa
isipokuwa Allah na kwamba Muhammad(SAW) ni Mtume Wake . Ameufikisha ujumbe,
ameituwa amana aliyopewa na akapigana Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu
kama alivyopaswa, basi Sala na Salam zimfikie Yeye na Aali na Masahaba wake
watukufu.
Amma Baad,
Hii ni tafsiri ya kitabu kilichoandikwa na Sheikh
Abdul Majeed Al Zindani akishirikiana na wanavyuoni wengine watano nao ni;
Abdullah Al Wadh-aaf
Ahmed Salama
Feisal Abdul Aziz
Hizam Al Bahluli
Tawhid Abdul Hameed
Kitabu hiki kwa lugha ya kiarabu kimepitiwa na
wanavyuoni mia moja, na majina
Hiki ni kitabu kilichojaa faida nyingi
Sheikh Abdul Majeed
Al Zindani ni miongoni mwa wanavyuoni wakubwa wa Kiislamu na
anajulikana
Hivi sasa (wakati wa kukifasiri kitabu hiki) yeye ni
Mkuu wa baraza la Shuura huko
Nilimpigia simu Sheikh Al Zindani na kuzungumza naye
kuhusu kukifasiri kitabu hiki kwa vile yeye ni mtungaji na mwenye haki za
kupiga chapa akanijibu;
"Vitabu vyangu vyote ni Wakfu kwa Waislamu wote, na
mimi sina haki yoyote ndani yake, nakuruhusu kukifasiri na kuuza tafsiri yako
unapotaka, isipokuwa tu usiwauzie ndugu zako kwa bei ya ghali'.
MUHAMMAD FARAJ SALIM
Hakika shukurani zote anastahiki Mwenyezi Mungu,
tunamuomba atusaidie katika shida zetu, atusamehe madhambi yetu, atukinge na
shari za nafsi zetu na shari za amali zetu ovu.
Atakaye Mwenyezi Mungu kumuongoza hakuna awezaye kumpoteza na anayeachiwa
basi hana uongofu.
Nakiri kwamba hapana apasaye kuabudiwa isipokuwa
Mwenyezi Mungu pekee asiye na mshirika, na ninakiri kwamba Muhammad (SAW) ni
Mtume wake na mjumbe wake.
Wa - baad,
Wajibu wa kwanza wa kila mwanadamu ni kumjua
Mwenyezi Mungu kwa njia ya Ilimu. Mwenyezi Mungu anasema :
"Juwa ya kwamba hapana Mola apasaye kuabudiwa kwa
haki isipokuwa Mwenyezi Mungu".
( Muhammad -
19 )
Wajibu wa pili ni kumjua Mtume wa Mola wake, na
ukweli wa ujumbe wake, kwa njia ya Ilimu inayompelekea kuwa na yakini.
Mwenyezi
Mungu anasema:-
"Jee anayejua kwamba yaliyoteremshwa kwako kutoka
kwa Mola wako ni haki (akayafuata basi) ni
( Al -
Raad -19)
Kila mwanadamu lazima aijue hikima (sababu) ya
kuumbwa kwake katika dunia hii, na ajue mwisho wa safari yake hii anayokwenda
na aijue Dini ya Mola wake ambayo ameamrishwa kuifuata".
Iwapo ubora wa Ilimu unajulikana kutokana na somo
lenyewe basi Ilimu ya Imani ni somo linalohusiana na kumjua Mwenyezi Mungu na
Mtume wake(SAW) na kuijua dini yake.
Na
Ushindi Juu Ya Maadui Zao. -
Mwenyezi
Mungu anasema :
"Na ni wajibu juu yetu kuwanusuru wale walioamini."
( Al-Ruum
- 47)
Kuwakinga.
-
Mwenyezi
Mungu anasema:-
"Hakika Mwenyezi Mungu huwakinga wale wanaoamini."
(Al - Hajj - 38)
Kuwalinda. -
Mwenyezi
Mungu anasema:
"Mwenyezi
Mungu ni Mlinzi wa wale walioamini."
(Al-Baqarah- 257)
Kuwaongoza. -
Mwenyezi
Mungu anasema:
"Na kwa yakini Mwenyezi Mungu ndiye awaongozaye wale
walioamini katika njia iliyonyooka."
(Al-Hajj - 54)
Kutoshindwa na Makafiri. -
Mwenyezi
Mungu anasema:
"Na Mwenyezi Mungu hatawajaalia makafiri njia ya
kuwashinda Waislamu."
(An- Nisaa - 141)
Kusimamisha Dini
Mwenyezi Mungu anasema;
"Mwenyezi Mungu amewaahidi wale walioamini miongoni
mwenu na kufanya vitendo vizuri kuwa atawafanya Makhalifa katika ardhi kama
alivyowafanya makhalifa wale waliokuwepo kabla yao, na kwa yakini
atawasimamishia dini yao aliyowapendelea na atawabadilishia
amani baada ya hofu yao "
(Al-Nur-55)
Riziki Njema .-
Mwenyezi
Mungu anasema :-
"Na lau
(Al aaraf 96)
Utukufu. -
Mwenyezi
Mungu anasema:-
"Na utukufu hasa ni wa MwenyeziMungu na Mtume wake
na wa Waislamu"
(Al Munafiqun-8)
Maisha Mema. -
Mwenyezi Mungu anasema :-
"Wafanyaji mema wanaume na wanawake, hali ya kuwa
wao ni Waislamu, tutawahuisha maisha mema "
(Al-Nahli-97)
Haya ni
baadhi ya mambo watakayopata Waislamu hapa duniani, na haya ndio waliyoyapata
wenzetu waliotangulia, walioamini kikweli.
Ama kuhusu Nyumba ya Akhera, Mwenyezi Mungu anasema:
"Kwa yakini walioamini na kufanya vitendo vizuri
makazi
(Al-Kahf -107-108)
Na akasema:
"Bila shaka wale walioamini na wakafanya vitendo
vizuri, zitakuwa kwao mabustani ya neema (peponi).Watakaa humo milele ni ahadi
ya Mwenyezi Mungu iliyo haki na Yeye ndiye Mwenye Nguvu (na) Mwenye Hekima."
(Luqman 8-9)
Anayechunguza hali za Waislamu leo, ataona kwamba
yale ambayo Mwenyezi Mungu amewaahidi Walioamini hapa duniani hawajayapata,
huu ni uthibitisho kwamba Imani zao ni dhaifu au wamepoteza sifa nyingi za
Imani, na hii ndio sababu ya kupoteza yale waliyoahidiwa na Mola wao hapa
duniani kama vile Ushindi juu ya maadui, Kuwakinga, Kuwalinda, Uongofu, Kuwa
Watukufu ulimwenguni, Kutoshindwa na makafiri, Riziki njema, Utukufu na Maisha
mema.
Atakayendelea na hali hii basi atayakosa hata yale
ambayo MwenyeziMungu amewatayarishia Walioamini, huko Akhera, na
Kwa hivyo lazima tuitie nguvu Imani, tuithibitishe
na kuiongezea nguvu mara kwa mara kwa njia ya kueneza Ilimu ya Imani baina ya
Waislamu, na kufuata Sheria za Dini.
Ni wajibu wa Ma-Ulamaa kujitolea na kusimamia wajibu
huu, hasa wakiwa wanaona namna wale wasioamini Mungu wakiwashambulia Waislamu
na kujaribu kuwaingiza katika dini zao, na pia wakiwa wanaona namna
zinavyoenea itikadi zisizo na msingi wa Kiislamu na mambo yaliyo batili ambayo
hao wanaoyaeneza wanajaribu kuyanasibisha maovu hayo na Uislamu.
Kwa hivyo kitabu hiki cha Imani tunakiweka mikononi
mwa Waislamu kikiwa ni miongoni mwa vitabu vinavyofunza wajibu wa Dini na
tunamuomba MwenyeziMungu akijaaliye kiwe ni kwa ajili Yake tu, na kiwafae
Waislamu .
Nasi tunamuomba kila mwenye kuionea uchungu Dini
yake afanye kila juhudi ili ajifunze na awafunze watu wake, jirani zake pamoja
na Waislamu wengine, na MwenyeziMungu ndiye anayefanikisha .
WATUNGAJI
IMANI NA UHAKIKA WAKE
MwenyeziMungu amekwishawabainishia waja wake Imani
gani inayokubaliwa na kuwafanya wayapate yale waliyoahidiwa na Mwenyezi Mungu
MýwenyeziMungu anasema;-
"Wenye kuamini kweli kweli ni wale waliomuamini
Mwenyezi Mungu na Mtume wake kisha wakawa si wenye shaka na wakaipigania dini
ya Mwenyezi Mungu kwa
(Al-Hujurat- 15)
Kutokana na aya hii, tunaona kuwa Imani inayokubaliwa
na iliyo ya kweli, ni itikadi isiyochanganyika na shaka, pamoja na kuipigania
Dini kwa mali na nafsi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.
Hii ni kwa sababu kuamini kwa moyo peke yake tu
hakutoshi kukubaliwa kwa Imani, kwani Iblisi alikuwa akiamini kuwepo kwa
Mwenyezi Mungu,
"Mola wangu nipe nafasi ya kuishi nisife mpaka siku
watakayofufuliwa viumbe".
(Sad 79).
Juu ya hayo, MwenyeziMungu amekwishampa sifa ya
ukafiri kwa sababu ya kutakabari kwake kwa kukataa kufuata amri ya Mola wake.
MwenyeziMungu anasema:-
"Isipokuwa iblisi akakataa na akajivuna na (tokea
hapo) alikuwa katika makafiri".
(Al- Baqarah-34).
Kwa Hivyo Imani Ya Haki Ni Ile Iliyokusanya yafuatayo:-
1)
Itikadi iliyo thabiti na
isiyokuwa na shaka.
2)
Matendo yanayosadikisha
Imani hiyo, nayo ni matunda yake.
·
Matendo ya Moyo, -
·
Matendo ya Ulimi, -
·
Matendo ya Kiwiliwili, - mfano wa Sala, Kutoa Zaka,
Kufunga, Kupigana Jihadi katika njia ya MwenyeziMungu, kutafuta Ilimu kwa
ajili ya Mwenyezi Mungu, kufanya biashara, kulima na kutengeneza vitu
viwandani ili kuihakikishia amri ya MwenyeziMungu ya kuwafanya watukufu
katilka ardhi kutokana na mafunzo ya Kiislamu.
Zipo sababu zenye kuzidisha Imani, -
MwenyeziMungu anasema:-
"Na wanaposomewa aya zake huzidi Imani".
(Anfal -2).
Na katika kumuasi Mwenyezi Mungu Imani inapungua.
Mtume (SAW) anasema:-
"Na wala hazini mzinifu wakati anapozini akawa yeye
ni mwenye Imani (Muumin)".
Na maana yake ni
'Pale mtu anapozini, huwa hana sifa ya Imani'.
Tukitaka kufanikiwa kuipata Imani ya kweli, hatuna
budi kuisimamisha Imani hiyo kwa njia zifuatazo:-
1)
Kuisadikishe nyoyoni kwa njia ya Ilimu
.
2)
Kutafakari katika
dalili za MwenyeziMungu zilizomo ulimwenguni na zilizomo katika Qurani,
pamoja na kujikumbusha ahadi aliyotupa MwenyeziMungu juu ya Pepo, pamoja na
maonyo (juu ya Moto).
3)
Matendo ya Ulimi , - Kama
vile kumtaja MwenyeziMungu sana, kutamka maneno ya haki na kulingania watu
katika njia ya MwenyeziMungu pamoja na kuamrisha mema na kukataza mabaya,
kujielimisha pamoja na kuelimisha na kuusiana katika kufuata haki na kuusiana
katika kushikamana na subira.
4)
Matendo ya viungo, -
MwenyeziMungu amesema :-
"Na ujiweke pamoja na wale wanaoabudu Mola wao
asubuhi na jioni, hali ya kuwa wanataka radhi Yake, wala macho yako yasiwavuke
(hawa ukawatafuta wengine) kwa kutaka pambo la maisha ya dunia wala usiwatii
wale ambao tumezighafilisha nyoyo zao wakafuata matamanio
Na sema "huu ni ukweli uliotoka kwa Mola wenu, basi
anayetaka na aamini na
anayetaka na akufuru".
(Al-Kahf 28-29).
Haya yote yanahitajia kuongoka kwa nyoyo na
kuzisafisha kutokana na maradhi
yanayomzuia mtu asipate hidaya ya Mola wake.
Mwenyezi Mungu anasema;
"Siku ambayo hayatofaa
(Al-Shuraa-88).
1)
KUIKUBALI HAKI.
Kuikubaili haki ni Jambo
linalompelekea mtu kuujua ukweli na kuufuata.
MwenyeziMungu amesema :-
"Habari njema (bushara
njema) ni zao.Basi wape habari njema waja wangu (hawa) ambao husikiliza kauli
nyingi zinazosemwa. Wakafuata zile zilizo njema . Hao ndio aliowaongoa
MwenyeziMungu na hao ndio wenye akili .
(Azzumar-17).
Ama nyoyo zilizokufuru-zenye
maradhi utaziona daima zinaipinga haki, hubaki na ujinga na wala haziongoki.
MwenyeziMungu amesema:-
"Na haiwafikii hoja yoyote
katika hoja za Mola wao ila wanakengeuka (wanaibishia).
(Al-An-Am - 4).
Mwenye moyo msafi daima huwa
anaipenda haki na anaupenda ukweli na moyoni mwake huipenda Dini na hutaka
kusoma juu ya Dini ya Kiislamu. Kwa hivyo mtu wa namna hiyo anaistahiki Hidaya
ya MwenyeziMungu.
Ama mwenye moyo ulio na
maradhi huichukia haki na huona dhiki kifuani pake anaposikia juu ya Uislamu.
Kwa ajili hiyo anajitakia mwenyewe adhabu ya MwenyeziMungu kutokana na
kujipotosha yeye mwenyewe.
MwenyeziMungu amesema:-
"Basi yule ambaye
MwenyeziMungu anataka kumuongoza, humfungulia kifua chake Uislamu; na yule
ambaye MwenyeziMungu anataka kumhukumu kupotea humfanya kifua chake kizito
kinaona taabu kubwa (kufuata huo Uislamu);
(Al-An-Am -125).
Na hii ni kwa sababu ya
kuichukia kwao haki.
MwenyeziMungu anasema:-
"Basi amewajia (Nabii
Muhammad ) kwa haki na wengi katika wao wanaichukia haki"
Al-Muumin - 70).
Mwenye moyo msafi huuitikia
mwito wa Imani,
"Mola wetu tumemsikia
mwitaji anayeita mwito wa Imani kwamba "Muaminini Mola wenu" Tukaamini, Mola
wetu tusamehe madhambi yetu na utusamehe makosa yetu na utufishe na watu
wema".
(Al-Imran - 193)
Mwislamu, siku zote hupenda
Imani yake izidi.
MwenyeziMungu anasema
:-
"Na inapoteremka sura (mpya
ya Qurani ) wako miongoni mwao (watu wanafiki) wasemao, "Ni nani miongoni
mwenu (sura hii) imemzidishia imani?" Ama wale walioamini inawazidishia imani
nao wanafurahi. Ama wale wenye ugonjwa nyoyoni mwao basi inawazidishia ubaya
(mpya) juu ya ubaya waliokuwa nao."
(Al -Tawba- 124-125).
Ama wenye nyoyo zenye
maradhi utawaona daima wanawazuilia watu njia ya MwenyeziMungu .
MwenyeziMungu anasema:-
"Wale wanaofadhilisha maisha ya dunia kuliko
akhera na wakawazuilia (watu) njia ya MwenyeziMungu na wanataka kuipotoa (na
hali ya kuwa si potofu) hao wamo katika upotofu (upotevu ) ulio mbali na
haki".
(Ibrahim - 3).
Wenye nyoyo safi utawaona
siku zote wanatafakari katika nafsi zao, na namna zilivyoumbwa mbingu na
ardhi, na wanatafakari katika uongofu
uliowajia kutoka kwa Mola wao, ukiwafahamisha hikima ya kuishi kwao na
ya kufa kwao, walikotokea na wanakoelekea pamoja na Pepo aliyowatayarishia
MwenyeziMungu waja wake walioamini, na adhabu inayowasubiri makafiri, na
wanatafakari juu ya miujiza ya Mtume (SAW) na juu ya ushahidi wa ukweli
aliokuja nao na jinsi ya kutekeleza yale aliyowaamrisha ili wajipatie furaha
ya dunia na ya akhera na ili wajiepushe na adhabu ya motoni.
MwenyeziMungu anasema:-
"Ambao humkumbuka
MwenyeziMungu wakiwa wima na wakikaa na wakiwa wamelala na hufikiri katika
kuumbwa mbingu na ardhi (wakasema) Mola, hukuviumba hivi bure utukufu ni wako
basi tuepushe na adhabu ya moto.
(Al -Imraan 191)
Lakini makafiri wameyafunga
masikio
MwenyeziMungu anasema juu
"Na watasema;
Binaadamu husahau, lakini
mwenye moyo msafi hukumbuka na kuiona njia.
MwenyeziMungu anasema :-
"Wale wanaomuogopa
MwenyeziMungu zinapowagusa pepesi za shetani (wakaasi) mara hukumbuka,
tahamaki wamekwisha ona njia".
(Al -Aaraf-201).
Ndio sababu MwenyeziMungu
akaamrisha kukumbushana, akasema;
"Endelea kuwakumbusha, maana
ukumbusho huwafaa wanaoamini."
(Al- Dharia 55).
Na akasema :-
"Basi waidhishe ikiwa utafaa
waadhi. bila shaka atakumbuka mwenye kumuogopa (MwenyeziMungu), na mwingi wa
mateso atajitenga nayo hayo (mawaidha) ambaye atauwingia moto mkubwa. Kisha
humo hatakufa wala hatakuwa hai"
(A -Alaa 10 - 13)
Ama wenye nyoyo zilizo na
maradhi utawaona wameghafilika wala hawaamini.
MwenyeziMungu amesema:-
"Na uwaonye siku ya majuto
wakati amri (ya kuingia Peponi na Motoni) itakapokatwa. Nao hapa duniani wapo
katika ghafla wala hawaamini"
("Maryam - 39 ).
Baadhi ya walioghafilika
unapowakumbusha juu ya siku ya kiama huenda wakakuambia;
"Unakuja leo kunifundisha
Uislamu? Mimi ni Mwislamu bora kuliko wewe".
Mwenye moyo msafi, mwenye kutafakari na kujielimisha
na Kujikumbusha utamuona keshaifikia Yakini
"Bila ya shaka katika mbingu na ardhi zimo alama
kubwa (za kuonyesha kuwa yupo MwenyeziMungu) kwa ajili ya wanaoamini. Na
katika umbo lenu na katika viumbe alivyovitawanya zimo alama (vile vile) kwa
watu wenye Yakini".
(Al - Jathiyah -3-4)
Ama yule aliyeghafilika, anayebisha utamuona siku
zote yumo katika shaka.
MwenyeziMungu anasema:-
"Lakini hao makafiri wamo katika shaka na wanacheza
tu".
(Al Dukhan -9).
Na wala hawaijui yakini isipokuwa
"Na ungaliwaona waovu wakiinamishwa vichwa vyao mbele
ya Mola wao, (Na kusema)
tumekwishaona na tumekwisha sikia basi turudishe tufanye vitendo vizuri,
hakika (sasa) tumeyakinisha (ungaliwaona katika hali hiyo ungaliwaona dhila
(As -Sajdah -12)
Wenye nyoyo
Ama makafiri nyoyo zao huwa ngumu na hazilainiki kwa
dalili zozote zile.
MwenyeziMungu anasema :-
"Je! Mtu ambaye MwenyeziMungu amemfungulia
(amemfungua) kifua chake kuukubali uislamu akawa yumo katika nuru itokayo kwa
Mola wake (ni sawa na mwenye moyo mgumu?) Basi adhabu kali itawathibitikia
wale wenye nyoyo ngumu wasimkumbuke MwenyeziMungu. Hao wamo katika upotofu
(upotevu) ulio dhahiri, MwenyeziMungu ameteremsha hadithi nzuri kabisa (kwa
kuteremshwa) kitabu chenye maneno yanayowafikiana, (yasiyopingana) na
yanayokaririwa (bila kuchosha) husisimka kwayo ngozi (miili) za wale
wanaomuogopa Mola wao, ikisha ngozi zao na nyoyo zao huwa laini kwa kumkumbuka
Mola wao."
(Az-Zummar -22-23)
Na
utawaona wenye nyoyo ngumu hizo wanajivuna na wanakuwa wakaidi pamoja na
kukanusha dalili za Mola wao.
MwenyeziMungu anasema :-
"Na wakazikanusha na hali ya kuwa nafsi zao zina
yakini nazo, wanazikanusha kwa dhulma na kujivuna”.
(Al - Naml -14).
Na hawa wanaotakabari wataadhibishwa.
MwenyeziMungu anasema:-
"Nitawaepusha na (kuzingatia) Aya zangu wale
wanaotakabari katika nchi pasipo na haki".
(Al -Aaraf 146).
Haya ni malipo
"Na (wakumbushe) siku watakapowekwa waliokufuru mbele
ya moto (waambiwe) mlipoteza vitu vyenu vizuri katika maisha yenu ya duniani
(basi hamtavipata leo hapa) Nyinyi
mlijifurahisha navyo (huko) basi leo mtapewa adhabu ya fedheha kwa sababu ya
kule kujivuna kwenu bure duniani na kwa sababu ya kule kuasi kwenu."
(Al - Ahqaf 20).
Utamuona mwenye moyo msafi
ni mtiifu wa Mola wake na kwa Mtume wa MwenyeziMungu na utamuona kila jambo
MwenyeziMungu anasema:-
"Wale wanaoamini wanaume na
wanawake, ni marafiki wao kwa wao. Huyaamrisha yaliyo mema na huyakataza
yaliyo mabaya na husimamisha Sala
na kutoa Zaka na humtii MwenyeziMungu na Mtume wake, hao ndio
MwenyeziMungu atawarehemu, hakika MwenyeziMungu ni Mwenye nguvu na Mwenye
hekima ".
(Al - Tawba -71).
Mtu wa aina hii huwa kesha
tii amri ya MwenyeziMungu isemayo:-
"Enyi mlioamini ! Mtiini
MwenyeziMungu na Mtume".
(An -Nisaa -59).
Na ile isemayo:-
"Na anachokupeni Mtume basi
pokeeni, na anachokukatazeni jiepusheni nacho, na muogopeni MwenyeziMungu, kwa
yakini MwenyeziMungu ni mkali wa kuadhibu".
(Al - Hashir -7).
Hii ni kwa sababu kumtii
Mtume (SAW) ni kumtii MwenyeziMungu.
MwenyeziMungu. Anasema:-
"Mwenye kumtii Mtume amemtii
MwenyeziMungu (kwani anayoamrisha Mtume yametoka kwa MwenyeziMungu)”.
Annisaa- 79
Ama mwenye moyo ulio na
maradhi utamuona akimfuata kila shetani
mwenye kuasi na hufuata matamanio yake na kujiabudia wengine wasiokuwa
MwenyeziMungu, huyo atakuja kujuta, lakini siku hiyo majuto hayatosaidia kitu
(majuto mjukuu).
MwenyeziMungu anasema:-
"Siku ambayo nyuso zao
zitapinduliwa pinduliwa (zitapounguzwa) Motoni watasema "Laiti tungemtii
MwenyeziMungu na tungemtii Mtume".
(Al -Ahzab -66).
Nyoyo zetu zikiwa na sifa
njema zilizotajwa hapo mwanzoni, ndipo tutakapokuwa miongoni mwa wenye nyoyo
Iwapo katika nafsi zetu
hatuoni amali njema, basi hii inatokana na udhaifu wa mti wa Imani uliomea
ndani ya nyoyo zetu na ambao haujatimiza sifa za moyo mwema.
Na iwapo hatutofanya haraka
kuzisafisha nyoyo zetu basi hali zetu hazitobadilika.
MwenyeziMungu amesema:-
"Hakika MwenyeziMungu
habadili yaliyoko kwa watu mpaka wabadili wao yaliyomo katika nafsi zao".
(Ar -Raad -11)
Na Mtume (SAW) amesema:-
'Ndani ya kiwiliwili mna
kipande cha nyama, kikitengenea, basi mwili wote hutengenea, na kikiharibika,
basi mwili wote unaharibika, kitu hichi ni moyo'.
Na moyo hautengenei
isipokuwa kwa kuongezeka Imani ndani yake na kuimakinisha.
Kumwamini MwenyeziMungu Ni Wajibu Wa Kila Mwanadamu
Mwanadamu akizingatia kidogo atagundua kwamba
MwenyeziMungu aliyemuumba amemjaalia viungo ili aweze kujielilmisha navyo
elimu zote za dini na za dunia, na bila ya vyombo hivyo hawezi kujielimisha
chochote.
MwenyeziMungu
amesema :-"Na MwenyeziMungu amewatoeni matumboni mwa mama zenu hali ya kuwa
hamjui chochote, na amekujaalieni masikio na macho na nyoyo ili mupate
kushukuru.
(Al -Nahli -78).
Jambo la mwanzo la kumshukuru MwenyeziMunguni ni
kuvitumia viungo hivi vya kujielimisha alivyotupa Mola wetu kwa ajili ya
kumjua Yeye.
MwenyeziMungu anasema:-
"Jua ya kwamba hakuna aabudiwaye kwa haki isipokuwa
MwenyeziMungu na omba maghfira kwa dhambi zako".
(Muhammad -19).
Bila ya kumjua Muumba wake,
binaadamu hawezi kuitambua na kuifuata njia ya Mola wake itakayompa furaha
hapa duniani na akhera, na kwa hivyo atakuwa miongoni mwa waliopata hasara.
Kwa ajili hiyo wajibu wa mwanzo kwa binaadamu ni kumjua MwenyeziMungu.
Mwanadamu akiitaka Imani iliyo sahihi, hana budi
kujielimisha.
MwenyeziMungu anasema:-
"Jee anayejua ya kwamba yaliyoteremshwa kwako kutoka
kwa Mola wako ni haki (akayafuata, basi) ni
(Ar -Raad - 9).
Hii ni kwa sababu Imani ya kuiga tu, (bila ya elimu)
hutetereka mara inapopambana na mtihani au inapopambana na mikanganyo (mambo
yanayobabisha).
Mwenyezi Mungu anasema:-
"Sema. Jee! wanaweza kuwa sawa wale wanaojua
na wale wasiojua? Wanaotanabahi ni wale wenye akili tu".
(Az - Zummar -9)
Na akasema:-
"Na katika watu wako wanaomuabudu MwenyeziMungu
ukingoni. Ikiwafikia kheri, hutuliya kwayo, na ikiwafikia fitina (msukosuko)
hubwatika juu ya uso wake (akasunukia hataki kuuona tena huo Uislamu) amepata
hasara ya dunia na akhera. Hiyo ndiyo hasara iliyo dhahiri".
(Al - Hajj -11).
Misingi Ya
Kiakili
ASIYEKUWEPO HAWEZI KUUMBA KITU.
Tukivizingatia viumbe vinavyozaliwa kila siku,
kuanzia binaadamu, wanyama na mimea, na tukitafakari juu ya kila kinachotokea
katika ulimwengu, mfano wa upepo, mvua, usiku, mchana, na tukitazama
yanayotokea kila wakati kwa mpangilio ulio na nidhamu, nidhamu ya jua na
mwezi, nyota na sayari, tukivizingatia hivi, pamoja na kuzingatia juu ya
mabadiliko yaliyojaa hekima yanayotokea ulimwenguni kila wakati, tutaona kuwa
akili ya mwanadamu huhakikisha kwamba vitu hivi havijaumbwa na ‘Asiyekuwepo’,
bali vimeumbwa na ‘Muumbaji’ ambaye ‘Yupo - Subhanahu wa Taala’.
MwenyeziMungu anasema:-
"Jee wameumbwa pasipo na kitu au wao ndio
waliojiumba. Au wameumba mbingu na ardhi?
(At -Tur -36).
Kila kilichokuwemo ndani ya
bidhaa yoyote kinafahamisha uwezo au sifa alizonazo yule aliyeitengeneza
bidhaa hiyo, na hii ni kwa sababu haiwezekani kuwepo kitu ndani ya bidhaa
ikiwa mtengenezaji hana uwezo au sifa za kumwezesha kukitengeneza.
Kwa mfano:-
Unapouona mlango wa mbao
umetengenezwa kwa ufundi kamili, utaelewa kuwa aliyeutengeneza anazo mbao, na
kwamba anao uwezo wa kuzikata kiasi atakacho (saizi aitakayo), pamoja na uwezo
wa kuzilainisha mbao hizo ziwe kama kioo (kwa kupiga randa), na utaelewa
kwamba anayo misumari na kwamba ni hodari wa kuziunganisha mbao hizo kwa
misumari.
Unapoiona tundu
iliyotobolewa kwa mpango maalum katika mlango huo, (kwa ajili ya ufunguo)
inatuthibitishia kwamba fundi huyo anao uwezo wa kuutoboa mlango kwa ustadi na
kwamba ana mpango ulio thabiti katika kazi yake.
Kwa njia hii tutaona kuwa
kila kitu kilichotengenezwa kinathibitisha uwezo na sifa alizonazo
mtengenezaji, maana haiwezekani kuwepo kitu katika
bidhaa isipokuwa mtengenezaji anao uwezo au sifa zinazomwezesha
kukitengeneza kitu hicho.
Kwa njia hii tunatambua kuwa
ukikichunguza chochote kilichotengenezwa utapata baadhi ya sifa za yule
aliyekitengeneza. Na kwa kufuata msingi huu tunaelewa kwamba tukivichunguza
viumbe tutapata baadhi ya sifa za Muumbaji.
MwenyeziMungu anasema:-
"Bila ya shaka katika mbingu
na ardhi ziko alama kubwa (za kuonyesha kuwa yupo MwenyeziMungu) Kwa ajili ya
wanaoamini na katika umbo lenu na katika viumbe alivyovitawanya zimo alama
(vile vile) kwa watu wenye yakini. Na katika kupishana (kufuatana) usiku na
mchana na katika riziki aliyoteremsha MwenyeziMungu kutoka mawinguni (mvua) na
akaifufua kwayo ardhi baada ya kufa kwake na katika mabadiliko ya upepo zimo
alama pia kwa watu wenye akili. Hizi aya za MwenyeziMungu tunakusomea kwa
ukweli basi hadithi gani watakayoiamini (baada ya kupuuza hadithi ya
MenyeziMungu na aya zake?")
(Al -Jathiya -3-6).
Tukichunguza na kutafakari
juu ya viumbe, vitatuelimisha juu ya alama za MwenyeziMungu ndani yake kwa
kutujulisha baadhi ya sifa Zake zilizomo ndani ya viumbe hivyo.
MwenyeziMungu anasema:-
“Sema’; tazameni nini
yanayotokea katika mbingu na ardhi".
(Younus -101).
Na akasema :-
"Jee hawatazami ufalme wa
mbingu na ardhi na vitu alivyoviumba MwenyeziMungu? (Hawatazami wakarejea kwa
Mungu kwa kuona) kuwa pengine ajali
(Al -Aaraf -185).
Chakula tulacho hakina uwezo
wa kusikia wala kuona wala hakitaharuki wala hakikuwi, hakivuti pumzi wala
hakioi, hakilali wala hakiamki. Kinapoingia mwilini, hubadilika kuwa sehemu ya
kiwiliwili kilicho na uhai na hubeba sifa zilizotajwa hapo mwanzo.
Pia katika mada mfano wa
maji, udongo, na hewa ambavyo ni vyakula vya mimea, vitu hivyo havikui wala
havizai wala havivuti pumzi wala havili chakula, lakini vinapoingia ndani ya
sehemu za miti hugeuka kuwa sehemu ya hiyo miti iliyo hai na
kusitawi.
Uhai huu unaoenea katika
kila kiwiliwili iwapo ni cha mti au mnyama au binaadamu kila siku na kila
wakati, unashuhudia kuwa umetengenezwa na Mtoaji wa uhai.
Binaadamu alijaribu
kuumba uhai akashindwa. Na wataalamu kutoka Mashariki na Magharibi ya
ulimwengu wamekwishatangaza kushindwa kwao kuumba uhai.
Na akasadikisha
MwenyeziMungu aliyesema:-
"Enyi watu! Unapigwa mfano,
basi usikilizeni; hakika wale mnaowaomba badala ya MwenyeziMungu hawawezi
kuumba (hata) nzi, wajapokusanyika kwa jambo hili. Na
(Al - Hajj -73-74).
Naam, na wanadamu
wanashindwa kukipata chochote alichokichukua nzi, na hii ni kwa sababu mara tu
baada ya kukichukua, hukitemea
mate na kukibadilisha haraka
Hakika uhai uliopulizwa na
unaoendelea kila wakati kupuliziwa viumbe hauwezi kupatikana isipokuwa
kutokana na Aliye Hai, Mwenye Kudumu milele (Subhanahu wa Taala).
Kila uhai
unatishwa na mauti kila inapokuja sababu ya kifo (
MwenyeziMungu amesema:-
"Ufalme wa mbingu na ardhi
ni wake. Anahuisha na kufisha, na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu."
(Al -Hadiyd -2).
Na akasema:-
"Na umtegemee (
MwenyeziMungu) wa milele ambaye hatakufa."
(Al-Furqan -58)
Ukikizingatia kiumbe chochote, utaona kuwa macho yake
yanaumbwa akiwa bado yumo ndani ya tumbo la uzazi la mama yake kabla
hajazaliwa, mahali penye kiza kizito, juu ya kuwa jicho halioni isipokuwa
penye mwangaza nje ya tumbo
Hata mbegu za miti MwenyeziMungu hutayarisha ndani
yake sehemu zitakazokuwa majani na matawi, na sehemu zitakazoingia ndani ya
ardhi (mizizi), ili iweze kunyonya maji na udongo (wenye chumvi chumvi).
Hawezi kufanya hayo isipokuwa Mwenye Kujuwa kwamba mti utahitajia maji na
udongo na mwangaza na hewa.
Viumbe vya kiume vikiumbwa,
utaona kwamba Muumbaji keshatayarisha idadi ya kike kiasi cha kutosheleza
idadi ya kiume. Hii inathibitisha kwamba hii ni kazi ya "Mjuzi" (Mwenye
Kujuwa) Subhanahu wa Taala.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na katika kila kitu
tumeumba dume na jike ili mpate kufahamu."
(Al -Dhariyaat 49).
Maji matamu yaliyotulia huharibika, lakini
MwenyeziMungu mwenye kuyaelewa hayo amejaalia maji ya bahari kuwa ya chumvi na
kuyafanya yawe na mawimbi ili kuwe na harakati na ili yasije maji hayo
yakaharibika na kuharibu maisha katika ardhi.
Haya, na yote yaliyomo katika ulimwengu huu yanashuhudia kuwa;
Muumba wa ulimwengu huu anakielewa kila anachokiumba.
Na Yeye ndiye aliyesema:-
"Oh! Asijue aliyeumba! naye ndiye avijuaye
visivyojulikana na vinavyojulilkana".
(Mulk -14).
Na elimu ya Mwenyezi Mungu imekizunguka kila kitu, haiguswi na ujinga
wala kusahau.
Mwenyezi Mungu amesema:-
"
(Al Talaq -12).
Ukizingatia sura za viumbe utaona kwamba Mwenyezi
Mungu ameviumba katika kila jinsi viumbe vilivyofanana (vyenye sura aina moja)
kwa hekima yake. Kwa mfano:-
Binaadamu ana macho mawili na pua baina ya hayo macho
na mikono ipo katika pande zake mbili na miguu ipo chini.
Hukuti jicho likawa gotini au mkono kutokeza juu ya
kichwa. Hii inathibitisha kwamba ni kazi ya Mwenye Hikima aliyeumba binaadamu
kwa hikima kubwa
Ameumba kila aina ya mnyama au mmea kwa hikima pia,
na ameviumba katika sura na mfano mmoja.
Ni nani basi aliyepanga sura hizi isipokuwa yule
aliyesema:-
"Yeye ndiye anaye kutengenezeni sura matumboni jinsi
apendavyo hakuna aabudiwaye ila Yeye Mwenye nguvu na Mwenye Hikima.
(Aali - Imran -6).
Ukiichunguza hewa tuivutayo utaona kwamba unaitumia hewa
Jee haithibitishi kwamba hii ni kazi ya Mwenye Kujuwa, Mwenye Hikima?
Ukiitazama pua yako utaiona imeumbwa kwa hekima ili ikubaliane na kazi
yake. Hewa huingia kupitia tundu mbili zilizopo baina ya macho, lakini Mjuzi,
Mwenye Hikima amezifunika tundu mbili hizo kwa ngozi ya pua, na akaijaalia
sehemu ya juu ya pua kuwa ni fupa ili upepo ukiwa mkali usije ukaibonyeza
nyama ya pua na kuzibana tundu za ndani ya pua ukashindwa kuvuta pumzi. Fupa
Lau kama pua yote ingelikuwa ni fupa tupu, basi tusingeweza kupenga kamasi.
Akajaalia pua iwe imepinda ili upepo unapoingia ndani uwe ukigonga
ukuta wa pua uliopinda na kuurudisha katika vikwazo vya ndani ili vigongane na
kugusana na vikwazo hivyo pamoja na kamasi zilizo kwenye mianzi ya pua na
kuvigandisha (kuzuwia) vijidudu (germs) pamoja na vumbi ili usafike upepo
kabla haujaingia ndani ya mwili.
(Upepo hauingii puani kuelekea katika mapafu moja kwa
moja).
Siku za baridi damu hujikusanya puani hata rangi ya pua hugeuka nyekundu ili
ipate kuupa joto upepo unapoingia. Ama siku za joto pua hufanya kazi ya
kuirowesha pua (jasho linapotoka) na kuuburudisha upepo mkavu au umoto
unaoingia.
Jee yote haya si ushahidi kwamba hii ni kazi ya Mwenye Kujuwa, Mwenye Hikima?
Na
hivi ndivyo ilivyo tukizingatia katika kuumbwa kwa kila kitu Ardhini au
Mbinguni tutagundua kwamba kimeumbwa kwa Hikima ya hali ya juu.
Hekima iliyo ndani ya kila kitu ni ushahidi kwa kila mwenye akili kwamba hii
ni kazi ya Mwenye Hikima, Mwenye Elimu, Utukufu ni wake Mwenyezi Mungu
aliyesema:
"Na Yeye
ndiye anayeabudiwa mbinguni na anayeabudiwa ardhini; Naye ni Mwenye Hikima,
Mwenye Elimu" .
Kizingatie vizuri chakula tunachokula. Ingawaje
kimetokana na udongo na maji namna moja, lakini vinapatikana ndani ya
mchanganyiko huo wa udongo na maji vyakula vya aina mbali mbali na vya rangi
mbali mbali. Hii inakuthibitishia kwamba hii ni kazi ya Mjuzi wa kila jambo,
ambaye kutokana na asili moja anatoa aina mbali mbali kwa Hikima ya hali ya
juu kabisa.
Zingatia jinsi gani kutokana na chakula hiki Mwenyezi
Mungu anavyoumba nyama, damu, mifupa, shahamu, maziwa, ngozi, nywele, vidole,
makucha, mishipa ya hisia na maji maji ya aina mbali mbali.
Kisha zingatia uso wako, jinsi gani mate hutokea
mdomoni na kamasi hutokea puani na machozi hutokea machoni na taka za masikio
kutokea masikioni, ingawaje vitokaji vyote hivi vinatokana na chakula kimoja,
ikikuthibitishia kwamba hii ni kazi ya Mwenye Ujuzi Subhanahu wa Taala.
Ingekuwaje kama mate yangetokea puani, na kamasi
zingetokea mdomoni? Taka za masikio zingetokea machoni, na machozi yakatokea
masikioni?
Nani aliyeuchagua mpango huu? Na nani aliyechagua
sehemu za kutokea? Hakuna mwingine isipokuwa yule Mwenye Elimu, Mjuzi, Mwenye
Hikima.
Na
tone ambayo kwayo Binadamu ameumbiwa, ameijaalia Mwenye Elimu, Mjuzi Suhanahu
wa Taala iwe na viungo mbali mbali na vyombo vilivyo na mpango vikishirikiana
kumhudumia binadamu.
Samaki baharini anahitajia hewa ili aweze kuvuta pumzi, Mjuzi akamyeyushia
hewa kisha akaiingiza pamoja na tone tone za mvua zinazoanguka baharini na
akamjaalia samaki awe na chombo maalumu (mashavu ya kuvutia pumzi) ili aweze
kuitumia hewa hiyo iliyoyeyushwa ndani ya maji.
Ukifikiri na ukichunguza vizuri utaona kwamba kila kitu katika ulimwengu
kimetengenezwa kwa ujuzi wa hali ya juu kabisa ikishuhudia kwamba hii ni kazi
ya Mjuzi wa kila kitu, Aliyetukuka Subhanahu wa Taala.
Mwanadamu anapokuwa amefungika ndani ya kiza cha tumbo la uzazi, hapana
yeyote anayeweza kumsaidia kwa chochote, si kwa maji wala kwa chakula. Hata
baba yake au mama ambaye ndani yake mwili huo unaumbika, pia hawawezi
kumsaidia isipokuwa kwa rehema yake Mtoaji wa Riziki ambaye humfikishia
chakula kikiwa kimewiva kimekwisha lainishwa kupitia kwenye bomba ambalo ni
kamba za kitovu (cha mama yake).
Mara
baada ya mtoto kuzaliwa kamba hizo hukatika, lakini Mtoaji wa riziki humtolea
chakula chake mtoto huyo kifuani pa mamake akiwa tayari keshajulishwa namna ya
kukitoa chakula hicho (maziwa) kwa kunyonya matiti wakati bado hajaanza hata
kuona, kusikia wala kufahamu.
Baada ya kukuwa MwenyeziMungu huwapa riziki viumbe vyake kutokana na mimea na
miti ambayo hutengeneza vyakula kutokana na maji, udongo na hewa.
MwenyeziMungu hulitiisha jua kwa ajili ya miti ili
ikamilishe kazi ya kutengeneza chakula ambacho huhitajiwa na binaadamu na
wanyama.
Chakula kisingeweza kupatikana lau
MwenyeziMungu anasema:-
"Hebu mwanadamu na atazame chakula chake, hakika sisi
tumemmiminia maji kwa nguvu kutoka mawinguni. Tena tukaipasua pasua ardhi,
kisha tukaotesha humo (vyakula vilivyo) chembe chembe. Na mizabibu na mboga na
mizeituni na mitende na mabustani (mashamba) yenye miti iliyosongana barabara.
Na matunda na malisho kwa ajili ya kukustarehesheni nyinyi na wanyama wenu."
(Abasa - 24 -32).
Mwanadamu au mnyama anapokula chakula na kusagika chakula hicho katika
mfumo wa kusaga chakula ambao MwenyeziMungu amemjaalia
kuwa nao kila kiumbe, basi Mtoaji wa riziki hiyo hukisambaza chakula
hicho kuelekea katika kila sehemu ya mwili wa kiumbe kilicho hai. Hukifikisha
mpaka katikati ya ubongo au sehemu ya chini ya ngozi au katika (ubongo wa
mafupa).
Na MwenyeziMungu amesadikisha alivyosema:-
"Au nani ambaye atakupeni riziki
(Almulk -21).
Mtoaji Riziki
Subhanahu wa Taala amekwisha dhamini riziki ya kila kiumbe, akapeleka riziki
ya samaki katika sehemu za chini kabisa za bahari, akaipeleka riziki ya baadhi
ya vijidudu na kukifikisha mpaka ndani ya mawe, akafikisha riziki za watoto
wachanga wakiwa ndani ya kiza cha matumbo ya uzazi ya mama zao, na
akakifikisha chakula cha mimea ndani ya mbegu.
MwenyeziMungu amesema:-
"Na hakuna mnyama yoyote (yaani kiumbe chochote)
katika ardhi ila riziki yake iko juu ya MwenyeziMungu. Na anajua makao yake ya
milele na mahali pake pa kupita tu (napo ni hapa duniani).Yote yamo katika
kitabu kinachodhihirisha (kila kitu)".
(Hud -60.)
Na akasema:-
"Enyi watu! Kumbukeni neema za MwenyeziMungu zilizoko
juu yenu. Jee yuko Muumba mwengine asiyekuwa MwenyeziMungu anayekupeni riziki
kutoka mbinguni na ardhini? Hakuna aabudiwaye kwa haki ila Yeye tu basi wapi
mnakopinduliwa".
(Fatir -3 ).
Mwenye yakini kwamba riziki yake inatokana na
Aliyemuumba, na kwamba yeyote hatoweza kumchukulia riziki yake, hatamwogopa
yeyote katika riziki yake isipokuwa MwenyeziMungu Peke Yake.
Ukizichunguza kope na nyusi, utaona kuwa nyusi zinaelekea juu na kope
zimeelekea chini. Ingekuwa kinyume cha hivyo (yaani nyusi zingeelekea chini na
kope kuelekea juu) mwanadamu
asingeweza kuona vizuri.
Ni nani basi anayeongoza kila unywele (wa nyusi na
kope na nywele nyengine) uelekee kila mmoja mahali pake
Nani mwenye kuyaelekeza meno ya chini yakaelekea juu
na ya juu kuelekea chini? Na nani aliyeyaongoza meno membamba ya mbele
yakachomoza mahali pake sawa sawa na meno ya pembeni mahali pake na magego
yakaota penye magego?
Ni nani
mwengine isipokuwa Mwenye Kuongoza?.
Mwenyezi Mungu anasema;
ý"Aliyeumba (kila kitu) na akakitengeneza na
akakikadiria (kila kimoja jambo lake) na akakiongoza (kufanya jambo
(A'laa -3-4ý)
Nani aongozaye
kila sehemu ya kiwiliwili katika mimea au wanyama au binaadamu mpaka kikawepo
mahali pake sawa sawa mwilini, kisha kikakuwa kwa kiasi kadiri inavyotakikana
kikikubaliana na mahali pake?
Nani mwenye kuiongoza mbegu ikaweza kupasua udongo
chini ya ardhi na kuelekea juu wakati inapomea na kuielekeza mizizi chini ya
ardhi, na vigogo pamoja na majani kuelekea juu? Kwa nini isipatikane hata
mbegu moja ikimea kinyume na hivyo?
Jee haya yote hayawi dalili kwa kila mwenye akili
kwamba hii ni kazi ya Mwenye Kuongoza – Al Haadiy Subhanahu wa Taala?
Nani anayeongoza majani ya miti yakagawika katika
sehemu mbali mbali za vigogo au katika matawi wakati linapochomoza jani upande
mmoja wa mti, jani lengine huchomoza upande wa pili?
Nani aliongozaye jua, mwezi na nyota katika njia zake
na akawaongoza ndege wanaosafiri kuelekea makwao mbali kabisa?
Ni Mwenye Kuongoza aliyesema:-
"Aliyeumba (kila kitu) na akakitengeza na
akakikadiria kila kimoja jambo
(Al - Aalaa -3-4)
Mwenyezi kukiongoza kila kitu, nywele na mbegu na majani, kisha akakamilisha
uongofu wake kwa binadamu kwa kumpelekea wajumbe (Mitume) ili kuwabainishia
uongofu utokao Kwake.
Mwenye yakini kwamba MwenyeziMungu ni Mwongofu na Mwenye Hikima,
hakubali fikra yoyote yenye kupingana na uongofu wake Subhanahu wa Taala, na
msemo wake siku zote huwa ile kauli ya MwenyeziMungu isemayo:-
"Sema uongozi khasa ni uongozi wa MwenyeziMungu".
(Al -An -Am -71).
Yule aliyekulinda na kila hatari huku ukiwa unaumbika
ndani ya tumbo la mama yako ndiye yule yule anayeulinda ubongo wako ulio
dhaifu akautia ndani ya kisanduku kigumu ndani ya fupa la bufuru la kichwa
chako, na ndiye Yule yule anayeyalinda macho yako kwa kuumba fupa la paji la
uso na ufupa wa paji la pua na mashavu, na ndiye anayeulinda moyo wako na
mapafu yako kwa kuizungushia mifupa ya kifua (mbavu).
Ni Yeye anayeulinda uhai wako na akakurahisishia
mahitajio ya kuishi mfano wa chakula, maji, hewa, mwangaza, joto na
venginevyo.
Ni Yeye ambaye hakupatishi tabu ya kui ingiza hewa
ndani ya mwili wako na kuitoa unapokuwa umelala au unapokuwa umacho. Lau kama
angelikukalifisha wewe kazi hiyo ya kuingiza na kuitoa hewa, basi usingekuwa
na wasaa wa kufanya jambo lolote lingine katika maisha yako yote isipokuwa
kuiingiza na kuitoa tu, na usingizi ukikuchukua ghafla, basi usingeipata hewa
na ukafa.
Hakika Mlinzi Subhanahu wa Taala ndiye anayeyaendesha
mawingu yaliyo juu yako, kisha hayamimini maji ya mvua yaliyojikusanya katika
mawingu hayo kwa wingi yakaangamiza mashamba na mimea, bali huyamimina kwa
njia ya mvua inayomwagika mfano wa maji ya marashi.
Hakika Mlinzi, (MwenyeziMungu) ndiye aliyeizungushia
dunia yetu (sayari "earth") mkanda wa hewa na michanganyiko mingine (Ozone
layer) unaozuia miale ya jua na ya nyota iangamizayo isiweze kutufikia
na kuangamiza maisha na kila kinachoishi, na akajaalia kuwepo mkanda
huo kuwa ni kinga yetu kwa kuviangamiza vimondo (shooting star), ambavyo
huangukia ardhini kwa mamilioni kila wakati usiku na mchana. Na Yeye ndiye
aliyeithibitisha ardhi isiweze kuyumbayumba chini ya miguu yetu kwa kuyaingiza
majabali ndani ya ardhi yakawa
Kwa nini basi tusimshukuru Mola wetu Subhanahu Wataala ambaye
ametuhifadhi ndani ya miili yetu na juu yetu na chini yetu?
MwenyeziMungu amesema kweli aliposema:-
"Ana (kila mtu) kundi (la Malaika) mbele yake na
nyuma yake wanamlinda (na kuyadhibiti anayoyafanya) kwa amri ya
MwenyeziMungu”.
(Al - Raad -11).
Na mwenye yakini kwamba MwenyeziMungu ndiye
anayemuhifadhi, basi hawezi kudhurika na yeyote yule awe yupo mbinguni au
ardhini isipokuwa kwa aliyekwisha kadiriwa na MwenyeziMungu, na msemo wake
siku zote ni kauli ya
MwenyeziMungu:-
"Sema "Halitotusibu ila alilotuandikia
MwenyeziMungu".
(At - Tawba -51)
Ukichunguza chakula kimoja kinacholiwa na ukoo mmoja, utaona kuwa
anapokula mwanamume hugeuka kuwa mwili wa kiume,
na chakula hicho hicho anapokila mwanamke hugeuka kuwa mwili wa kike,
na katika mwili wa mtoto hugeuka mtoto na anapokula chakula hicho hicho paka,
basi hugeuka kuwa mwili wa paka. Anapokula panya au mbwa hugeuka kuwa ni
sehemu ya mwili wa panya au mbwa, wakati chakula ni hicho hicho kimoja, basi
Utukufu ni wake Mwenye Kutengeneza sura
Na ukiichunguza huruma ya mama na namna anavyowaonea
huruma wanawe, yote sawa iwapo mama huyo ni mwanadamu au mnyama, utamauona
namna gani anavyojitolea mhanga kwa ajili ya kuwalinda wanawe.
Hata kuku ambaye kwa kawaida huogopa hata sauti ya
mtoto mdogo, utamwona namna anavyokasirika na kumshambulia yeyote anayejaribu
kuvidhuru au hata kuvisogelea vifaranga vyake.
Hakika rehema hizi ambazo hujaaliwa kuwa nazo hata viumbe vidogo
vidogo, ni ushahidi mkubwa kuwa hii ni kazi ya Mwenye Kuneemesha neema ndogo
ndogo na Mwenye Kuneemesha neema kubwa kubwa Mwingi wa Rehma.
Ukivichungua viumbe vikubwa
Hapo ndipo utakapo pata jibu kwamba hii ni kazi ya
Mwenye Nguvu, Mwenye kuyaendesha Mwenyewe mambo Yake, Subhanahu Wataala.
Kila kitu duniani kinashuhudia kwamba kimeumbwa na
Mmoja tu Aliye Pekee.
Chakula chako kwa mfano, hutegemea kazi ya tumbo (kwa
usagaji wa chakula). Na madaktari wanasema kuwa usagaji wa chakula unategemea
mzunguko wa damu, na damu ili ifanye kazi yake vizuri huitegemea hewa na
uvutaji wa pumzi, na ili ipatikane hewa safi inategemea kazi ya miti (ambayo
ndiyo inayoisafisha hewa hiyo), na ili miti iweze kufanya kazi yake sawa
inalitegemea jua, na jua ili libaki linazitegemea sayari zilizoizunguka pamoja
na nyota nyengine.
Kwa hivyo utaona kwamba kila kitu ili kiwepo na ili
kiweze kufanya kazi yake vizuri, kinategemea kitu kingine.
Hii inathibitisha kwamba kila kitu kimeumbwa na Mungu
Mmoja.
MwenyeziMungu anasema:-
"MwenyeziMungu hakujipatishia mtoto wala hakuwa
pamoja naye mungu (mwengine). Ingekuwa hivyo basi kila mungu angaliwachukuwa
aliowaumba. Na baadhi
(Al -Muumin -19)
Na akasema:-
"Sema; "Yeye ni MwenyeziMungu ni Mmoja (tu).
MwenyeziMungu tu ndiye anayestahiki kukusudiwa (na viumbe vyake vyote kwa
kumuabudu kumuomba na kumtegemea) hakuzaa wala hakuzaliwa".
(Ikhlas -1-3)
Na
MwenyeziMungu anasema:-
"Lau kwamba wangalikuwepo humo (mbinguni na ardhini)
waungu wengine isipokuwa MwenyeziMungu, bila shaka zingeharibika (hizo mbingu
na ardhi). Na ametakasika MwenyeziMungu Mola wa Arshi (yu mbali) na yale
wanayomsifu."
(Al -Anbiyaa -22)
Kutokana na yaliyotangulia tumeona kuwa unapotafakari juu ya ulimwengu na
viumbe tunavyoishi navyo, utagundua kuwa Muumba wa vitu hivi ni Muumbaji,
Aliye Hai, Mwenye Ujuzi, Mwenye Kutoa Riziki, Mwenye Kuongoza, Mlinzi,
Mtengenezaji wa sura, Mwenye Kurehemu, Mwenye Nguvu, Mwenye Uwezo, Mmoja tu
Aliye Pekee.
Na
"ASH - HADU AN LAA ILAAHA ILLA LLAH"
"Nashuhudia kwamba hapana Mola apasae kuabudiwa
isipokuwa Mwenyezi Mungu".
Na iwapo katika
msingi wa mwanzo tumeelewa kwamba ASIYEKUWEPO HAWEZI KUUMBA KITU, na
katika na msingi wa pili tukazielewa BAADHI YA SIFA ZA MUUMBAJI.
Basi katika msingi wa tatu tutaelewa kwamba
sifa hizi hazimfai yeyoye yule isipokuwa (ALLAH), MwenyeziMungu Asiye na
mshirika.
Asiyekua na mali watu
hawamuombi mali, na asiyekuwa na elimu hawezi kuelimisha, na hii ni kwa sababu
asiye na kitu hawezi kutoa (KWA SABABU HANA KITU).
Kwa
kuyazingatia haya tumepata dalili na ushahidi katika kila kiumbe
inayotujulisha baadhi ya sifa za Muumbaji - Subhanahu wa Taala. Na
tunapotambua sifa, tunamjua mwenye sifa hizo.
Sasa wale wanaodai kuwa
maumbile ndio yaliyowaumba, wamekwenda kinyume na akili na wameupiga vita
ukweli, na hii ni kwa sababu ulimwengu wote unashuhudia kwamba aliumba ni
Mwenye Hikma, Mwenye Ilimu, Mwenye Ujuzi, Mwenye Kuongoza, Mtoaji wa Riziki,
Mlinzi, Mwenye Kurehemu, Mmoja Aliye Pekee.
Hayo maumbile
yasiyoweza kusema, yaliyokauka, yasiyokuwa na elimu wala hikima, hayana uhai
wala rehma wala uwezo, vipi basi
wajinga wakawaza namna hii (kuwa hayo ndiyo yaliyowaumba?)
wakati ASIYEKUWA NA KITU HAWEZI KUTOA.
Maumbile ni hivi viumbe
pamoja na sifa zinazobeba. Wanaoabudu viumbe toka zamani waliabudu baadhi ya
viumbe
Na hawa wanaoabudu viumbe wa
siku hizi (wana wa maumbile) wanadhania kuwa vitu hivi vilivyokuwa vikiabudiwa
hapo zamani (maumbile) kuwa ndiyo vilivyowaumba, wakati ambapo maumbile hayana
hata akili na wao wanazo akili, maumbile hayana ilimu, na wao wanayo ilimu!!!
Maumbile hayana ujuzi wao wanao
ujuzi !!! maumbile hayana uwezo na wao waonao uwezo.
Jee hawaelewi kuwa
ASIYEKUWA NA KITU HAWEZI KUTOA?
MwenyeziMungu amesema:-
"Enyi watu unapigwa mfano
basi usikilizeni hakika wale mnaowaomba badala ya MwenyeziMungu hawawezi
kuumba hata nzi japo wakikusanyika kwa jambo
Amedhoofika kweli kweli huyu
mtaka (kupokonya) na mtakwa (kupokonywa).
Hawakumuadhimisha
MwenyeziMungu kama anavyostahiki kuadhimishwa hakika MwenyeziMungu bila shaka
ni Mwenye nguvu na Mwenye kushinda."
(Al - Hajj -73-74).
Baadhi ya wasioamini
MwenyeziMungu wanadai kuwa eti maumbile ndiyo yenye kuumba wakitegemea
ushahidi wao juu ya kutokeza kwa vijidudu (funza n.k) kutokana na takataka na
mizoga ya wanyama na maiti ya wanadamu.
Elimu iliposonga
mbele ikawaelimisha watu kwamba wadudu hawa wanaotokeza penye mizoga na sehemu
nyingine wanatokana na mayai madogo
Kisha wakadai tena kwamba
eti ikiwa vijidudu hivyo vinatokana na vijidudu vingine vilivyotangulia
vilivyotokana ndani ya vijiyai vidogo ambavyo hatuvioni, basi germs ambao
husababisha chakula kuoza na kuharibika wanatokana na maumbile na kwamba
hawatokani na vijidudu vingine vilivyokuwepo kabla
Lakini madai haya pia
yakashindwa kiasi cha miaka Themanini iliyopita wakati watalamu walipogundua
njia ya kuhifadhi chakula bila ya kuharibika kwa kuviingiza kwa ustadi ndani
ya makopo, na vijidudu vikafa kwa joto la kupikwa au miale ya joto kisha
kikafunikwa kwa ustadi ili hewa (inayobeba vijidudu hivyo) isiweze kuingia
ndani na kusababisha kuingiza vijidudu wengine.
Kwa njia hii ikajulikana
kuwa viumbe vyote vinatokana na viumbe vilivyokuwa kabla
Utashangaa ewe Mwislamu, kwamba miongoni mwa viongozi wasioamini kuwepo kwa
MwenyeziMungu wanayajua haya tokea miaka themanini iliyopita, lakini
wanashikilia kueneza habari hizo za kijinga za kutoaamini Mungu ambazo
hazidumu ila na wajinga.
MwenyeziMungu alipomwokoa
Nabii Issa (AS) kutokana na vitimbi vya maadui wake na kumnyanyua kwake,
maulamaa wa Kinasara waliobaki waliingizwa katika vitisho vya Warumi, na wengi
wao wakatoweka na wengine wakauawa na
ujinga ukaenea baina ya Manasara.
Injili ya Nabii Issa
(AS) ikapotea, wakaibadilisha kwa Injili walizozitunga wao wenyewe na kila
mtungaji akaandika jina
Kisha ukafanywa mkutano wa
Manasara wakazichagua nne tu miongoni mwa hizi Injili na kuziunguza
zilizobaki.
Kisha wakadai kwamba
MwenyeziMungu amegawika sehemu tatu na kwamba Issa ni mwana wa Mungu, wakati
MwenyeziMungu yuko mbali juu kabisa na hayo wanayomsingizia.
Kisha baadaye wakasema
kwamba MwenyeziMungu ni mmoja lakini wakaanza kuamini mambo yasiyoingia
akilini nayo ni kwamba Mungu ni mmoja lakini wakati huo huo ni watatu
(amegawika sehemu tatu).
Mshairi maarufu Albusiyri, alisema:-
"Wamefanya watatu kuwa ni
mmoja, lau wangeongoka wasingeweza kuifanya idadi kubwa kuwa moja".
Kisha wakadai kwamba mungu
(Nabii Issa(AS), amekufa msalabani, - ingawaje wanaamini kwamba Malaika hawafi
- na kwamba binaadamu (Mayahudi na Warumi) ndio waliomuuwa. Injili
Na MwenyeziMungu anasema:-
"Hawakumuua wala
hawakumsulubu bali walibabaishiwa na kwa hakika wale waliokhitilafiana katika
(hakika) hiyo wamo katika shaka, hawana yakini juu ya hili isipokuwa wanafuata
dhana tu. Na kwa yakini hawakumwua bali MwenyeziMungu alimnyanyua kwake na
MwenyeziMungu ni Mwenye Nguvu na Mwenye Hekima."
(Al -Nisaa - 157-158).
Kuhusu madai
MwenyeziMungu anasema:-
"Bila ya shaka hali ya Issa
kwa MwenyeziMungu ni
Aal -Imran -59).
MwenyeziMungu amekwisha
bainisha kuwa Issa (AS) ni mwanaadamu na alikuwa akila chakula, na anayekula
hana budi kufanya haja (ndogo na kubwa).
Vipi basi awe Mungu yule
ambaye hana budi kula, kunywa na kufanya haja?
MwenyeziMungu anasema:
"Masihi bin Maryam si
chochote ila ni Mtume, bila shaka Mitume wengi wamepita kabla yake na mama
yake ni mwanamke mkweli. Wote wawili walikuwa wakila chakula. Tazama jinsi
tunavyobainisha aya, kisha tazama jinsi wanavyogeuzwa".
(Al -Maidah- 75).
Kila mtu anaweza kumjua
Mungu wake kwa urahisi kwa njia ya kuona jinsi dua inavyojibiwa. Mara ngapi
Waislam walitoka kwa nyoyo tiifu, zilizotubu, wakimuomba Mola wao awanyeshee
mvua, na majibu ya dua zao hupatikana hapo hapo?’ Mvua hunyesha katika kijiji
au mji, mahali ambapo watu walitoka wakimuomba MwenyeziMungu awaletee hiyo
mvua wakati ambapo vijiji na miji ya jirani haipati mvua hiyo. Wangapi
waliokuwa na dhiki wakapata faraja baada ya kumuomba Mola wao?
MwenyeziMungu amesema:-
“Áu yule anayemjibu
aliyedhikika amwombapo na kuondoa dhiki yake na kukufanyeni wenye kuendesha
dunia. Jee yupo Mungu pamoja na MwenyeziMungu? Ni kuchache kuwaidhika kwenu."
Dalili za imani juu ya
kuwepo kwa MwenyeziMungu ni nyingi, na idadi yake ni sawa na idadi ya viumbe
vyote vilivyopo duniani, kwa sababu kila kiumbe kinatujulisha sifa za Muumbaji
wake. Lakini makafiri hawajanufaika na dalili hizi kwa sababu nyoyo zao zina
maradhi, haziko tayari kuyakubali maongozo,
kinyume na nyoyo zilizoamini.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na katika watu wako
wanaojadiliana juu ya MwenyeziMungu bila ilimu wala uongozi wala kitabu chenye
nuru."
(Al - Hajj -8).
Utamwona pia akizifanyia
kiburi dalili za MwenyeziMungu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na wakazikanusha hali ya
kuwa nafsi zao zina yakini nazo (kuwa ni kweli, lakini walizikanusha) kwa
dhuluma na kujivuna."
(An - Naml -14)
Na utamwona anachanganya
haki na batili.
MwenyeziMungu anasema:-
"Wala msichanganye haki na
batili na mkaficha haki na hali mnajua."
(Al
-Baqarah -42)
Na utamwona anazuia watu
wasifuate njia ya MwenyeziMungu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Hakika wale waliokufuru na
kuzuilia (watu) njia ya MwenyeziMungu bila shaka wamepotea upotofu ulio mbali
(na haki)."
(An - Nisaa -167).
Miongoni mwa sifa za ukafiri
ni kwamba wakati wanaikataa Imani juu ya kuwepo kwa dalili zilizo wazi, badala
yake wanaielekea (wanaikubali) kufru bila ya dalili yoyote, wanafuata tu mfano
wa kipofu.
Mwenyezi Mungu anasema;
"wanapoambiwa 'Njooni katika
hukumu alizoziteremsha MwenyeziMungu na (anazozisema) Mtume, husema
yanatutosha yale tuliyowakuta nayo baba zetu'. Jee hata
(Al - Maidah -104).
Miongoni mwa vitimbi vya
makafiri katika kutaka kuwapoteza Waislamu ni kuzusha mambo yanayobabaisha
yanayoweza kumpoteza asiyeielewa Itikadi yake na asiyejijengea ngome (ya ilimu
ya dini yake) kwa ajili ya kujilinda na ubabaishaji wa wale wasioamini Mungu.
Miongoni mwa maneno
wanayoyatumia ni yale waliyosema wana wa Israil (tokea zamani) kumwambia Musa
(AS),
"Na mliposema "Ewe Musa!
hatutakuamini mpaka tumwone MwenyeziMungu wazi wazi".
(Al - Baqarah - 55)
Ingawaje makafiri hao
wanaamini kuwepo kwa akili inayoweza kufikiri, kuwepo kwa hewa, na kuwepo kwa
nguvu ya mvutano inayovuta kila kitu kuelekea ardhini na wanaamini kuwepo kwa
mawimbi ya sauti yanayowafikia kutoka sehemu za mbali, juu ya kuwa vyote hivyo
hawavioni kwa macho yao, lakini wanaiona athari ya akili kutokana na wenye
akili na wanaiona athari ya hewa kutokana na kutikisika kwa matawi ya miti na
venginevyo, na athari ya nguvu ya mvutano inaonekana kutokana na kuvutika kwa
kila kitu kuelekea ardhini, na wakaamini kuwepo kwa mawimbi ya sauti baada ya
kuiona athari yake kwa njia ya sauti zinazosikika kutoka kwenye vyombo vya
idhaa n.k.
Kwa hivyo wameamini kuwepo
kwa akili, hewa na nguvu za mvutano juu ya kuwa macho yalishindwa kuviona kwa
udhaifu wake, lakini akili ikatambua kutokana na athari zake walizozishudia.
Laiti wale wasioamini
wangeacha kutakabari na hizo nguvu zao za kuona zilizo dhaifu, zisizo na
uwezo, zisizoweza kuiona hewa wanayoigusa au kukiona kitu kilichokuwepo nje ya
pale walipo. Wangelitafakari wangeligundua kwamba wao pamoja na vilivyomo
ulimwenguni, zikiwemo ardhi na mbingu, si chochote isipokuwa ni dalili na
ushahidi ulio wazi ukiwajulisha kuwepo kwa Muumba wao Subhanahu Wa Taala.
Uwezo huu wa kuona ulio
dhaifu hauna nguvu ya kuziona nyota kwa ukamilifu. Nyota ambazo ni pambo tu la
mbingu ya dunia, vipi basi wataweza kumuona Yule Aliye juu kabisa kwenye Arshi
Yake?
(Mbingu zote saba zikilinganishwa na
kiti Chake (Mwenyezi Mungu) ni sawa na senti ndogo saba ukizitia ndani ya ngao
(ya kujikingia katika vita). Na Kiti kikilinganishwa na Arshi Yake
MwenyeziMungu ni mfano wa pete ndogo iliyotupwa jangwani).
Iwapo macho ya binaadamu
katika dunia hii hayawezi kuvumilia kulitazama jua moja kwa moja, vipi basi
yatakuwa na uwezo wa kuiona Nuru ya MwenyeziMungu Aliyetukuka, Aliye juu ya
yote?
MwenyeziMungu
angejidhihirishia kwa viumbe vyake duniani, basi kujidhihirisha huko
kungeliwalazimisha watu kumfuata, na huko kungeifanya dunia isiwe mahali pa
kufanyiwa mtihani maana kumuamini Mungu wakati huo kungekuwa ni kwa njia ya
kulazimishwa na kwa hivyo pangeondowa ile maana ya Majaribio au Mtihani.
Nabii Mussa(AS) hapo zamani
alimwomba amuone Mola wake.
MwenyeziMungu anasema:-
"Basi Mola wake
alipodhihirisha baadhi ya Nuru Yake katika jabali alifanya lenye kuvunjika
vunjika na Musa akaanguka hali ya kuzimia ".
(Al
Aaraf -143).
Watu wote wakiwemo makafiri,
wanawasadiki madaktari na wenye ujuzi pamoja na walimu wanapowaeleza juu ya
mambo wasiyoweza kuyaona kwa macho
Basi hao makafiri wangeacha
kiburi chao, wao pia wangelimjua Mola wao kwa njia ya kuwasadiki Mitume wa
MwenyeziMungu wasemao kweli, ambao kwa miujiza na ushahidi waliokuja nao
unawafanya kuwa ni watu wanaofaa kusadikiwa zaidi kupita wote duniani kutoka
na wanayoyasema juu ya Mola wao.
Wapo wengine wanaomwekea
masharti MwenyeziMungu ili wamuamini.
Utawasikia wakisema kwa
mfano;
"Iwapo Mungu anataka
nimuamini, basi afanye hiki au kile". Na huu ni mfano wa makafiri uliotajwa
katika Qurani:-
"Na walisema (makafiri wa
kikureshi kumwambia Mtume) hatuwezi kukuamini mpaka utububujishie
(utupitishie) chemchemu katika ardhi. Au uwe na bustani ya mitende na mizabibu
ikisha ububujishe
Israa( Bani Israil) 90 - 92.
Na
MwenyeziMungu anasema:-
"Na kama "Haki"
(MwenyeziMungu) angefuata matamanio yao, zingeliharibika mbingu na ardhi na
vilivyomo ndani yake".
(Al Muumin - 71
MwenyeziMungu amesimamisha
dalili nyingi katika viumbe vyake, na akatupa uwezo wa kusikia na kuona,
akatupa nyoyo ili tuweze kuzijua dalili hizo na kwa njia hii ukweli unasimama
na kubabaika kunaondoka.
Umuhimu Wa Kuyajua Majina
Yake Na Sifa Zake
Unapoambiwa kuwa mtu fulani
ni karimu na kwamba moja kati ya sifa zake ni kumpa kila muhitaji, bila shaka
unapokuwa na shida utategemea kupata uyatakayo kutoka kwake, na utamheshimu
mtu huyo moyoni mwako kwa kuwa yeye ni mkarim, na utafaidika kutokana na
kuijua sifa yake hii ya ukarimu pale unapohitaji.
Na kinyume chake pale
unapoelewa kuwa mtu ni bakhili, (Hutotegemea kuyapata mahitajio yako kutoka
kwake kwa sababu ya ubakhili wake wa kuogopa kupungukiwa na mali yake).
Unapoambiwa kuwa serikali
fulani ina uadilifu katika kuhukumu kwake na kwamba inawashughulikia wanaoishi
ndani ya nchi hiyo na kuwatia adabu wasiofuata kanuni, watu watamiminika
katika nchi hiyo ili wafaidike na sifa za huduma zake pamoja na kufaidika na
sifa ya uadilifu wake na sifa ya kuiheshimu kwake sheria. Utawaona watu hao
wanaipenda serikali hiyo kutokana na sifa njema iliyo nayo, huku wakijaribu
kila njia kujiepusha na kuvunja sheria ili wasije wakahukumiwa na kutiwa
adabu.
MwenyeziMungu ndie mwenye
sifa tukufu zaidi. Kwa mwenye kuzijua sifa za Mola wake na majina Yake mazuri
mazuri, elimu yake juu ya MwenyeziMungu Mwenye Ufalme wa mbingu na ardhi
inaongezeka, na mwenendo wake huwa unalingana na elimu aliyonayo juu ya Majina
na Sifa za MwenyeziMungu.
Ama makafiri, MwenyeziMungu
amesema juu yao yafuatayo:
"Hawakuamuadhimisha
MwenyeziMungu kama anavyostahiki kuadhimishwa. Hakika MwenyeziMungu bila shaka
ni Mwenye Nguvu Na Mwenye Kushinda”.
(Al -Hajj 74)
Na Qurani imetuhadharisha
juu ya kubadilisha majina ya MwenyeziMungu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na MwenyeziMungu ana majina
mazuri mazuri basi muombeni kwa hayo. Na waacheni wale wanaoharibu utakatifu
wa majina yake karibuni hivi watalipwa yale waliokuwa wakiyatenda ."
(Al -Aaraf -180)
Qurani pia imekwisha onya
juu ya kumpa MwenyeziMungu sifa zisizolingana Naye.
Mwenyezi Mungu anasema;
"MwenyeziMungu
hakujipatishia mtoto wala hakuwa pamoja
naye mungu (mwengine). Ingekuwa hivyo basi kila Mungu angewachukua
aliowaumba, na baadhi yao wangeliwashinda wengine. MwenyeziMungu ameepukana na
sifa wanazomsifu nazo (zisokuwa ndizo)."
(Al -Muumin 91.)
Elimu ya mwanadamu juu ya
viumbe vya MwenyeziMungu ina mpaka wake na mwanadamu hawezi kujua kila kitu
juu ya Mola wake.
Kwa mfano mbingu zote saba
zikilinganishwa na Kiti Chake MwenyeziMungu, ni sawa na senti ndogo saba
ukizibandika juu ya ngao kubwa, na hicho Kiti ukikilinganisha na Arshi ya
MwenyeziMungu ni sawa na pete ndogo iliyotupwa jangwani.
(Mwenyezi Mungu anacho Kiti
(Kursy) na anayo Arshi - hivi ni vitu viwili tofauti , na Arshi ni kubwa sana
kuliko Kiti).
MwenyeziMungu anasema:-
"Ndiye Mungu mwenye rehma
aliyetawala juu ya Ashi yake".
(Taha -5).
Ilimu yetu haiwezi
kuizizunguka na kuzijua nyota ambazo ni pambo la mbingu ya dunia, kwa hivyo
hatuna uwezo wa kuizunguka kwa kujua kila kitu juu ya Mola wetu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Wala hawalijui lolote
katika elimu yake ila alipendalo. Enzi yake imeenea mbingu na ardhi wala
kuvilinda hivyo hakumshindi na Yeye peke Yake ndiye Aliye juu na ndiye Aliye
Mkuu."
(Al -Baqarah -255).
Kwa hivyo sisi wanadamu
hatuna ilimu ya kutuwezesha kumjua Allah kama alivyo, isipokuwa kwa ilimu
itokayo kwake, na kwa vile umekwishatujia kutoka kwa MwenyeziMungu ubainifu na
ilimu, na Akatujulisha juu Yake na juu ya sifa Zake, kwa hivyo tusimame hapo
hapo bila ya kuongeza mengine kutoka kwetu, na tumtukuze MwenyeziMungu kwa.
Inaposemwa kwamba; "Mfalme
fulani ni karimu na mlinzi wake ni karimu na mwanawe ni karimu", Bila shaka
asikiaye hayo atatofautisha baina ya ukarimu wa mfalme, ukarimu wa mlinzi, na
wa mtoto wa mfalme ingawaje wote hao ni wanaadamu.
Na utakapoambiwa kuwa;
"MwenyeziMungu ni Karimu", bila shaka utajuwa kuwa ukarimu wake MwenyeziMungu
aliyetukuka haufanani hata kidogo na ukarimu wa viumbe vyake
alowamiliki na walio dhaifu.
Hivi ndivyo ilivyo katika
sifa zake zote MwenyeziMungu Subhanahu wa Taala.
Elimu Yake ni tofauti na
elimu ya viumbe vyake, na Hikima Yake inatofautiana na hikima ya viumbe vyake
na Rehema Zake juu ya walioamini na Ghadhabu Zake juu ya waliokufuru ni
tofauti na rehema na ghadhabu za viumbe vyake. Vyote hivyo na venginevyo Yeye
amekamilika navyo ukamilifu wa hali ya juu kabisa usio na mfano wowote;
MwenyeziMungu anasema:-
"Hakuna chochote mfano wake
nae ni mwenye kusikia, na mwenye kuona."
(Al-Shuraa 11)
Kwa hivyo upungufu
unapatikana kwa asiyekuwa Yeye, ama Yeye (MwenyeziMungu) Pekee ndiye
Aliyekamilika.
Miongoni mwa fadhila za
MwenyeziMungu juu yetu ni kwamba kwa Ilimu Yake na kwa Hikima Yake
ametujulisha ni nani Yeye, ametufundisha hayo kupitia katika kitabu chake na
katika mafundisho ya Mtume wake (SAW). Akatujulisha kwamba ana majina yaliyo
bora kabisa na sifa za ukamilifu, na kwamba haiwezekani kwa Mwislamu
kubadilisha katika sifa alojipa Mwenyewe Subhanahu Wataala.
Mwanamke mmoja wa
kizungu ambaye mumewe ni Mwislamu alikwenda kujadiliana na Sheikh Al Hakim.
Huyu ni Sheikh aliyemsilimisha mumewe bibi huyo.
Majadiliano yalikuwa kama
yafuatavyo:-
Bibi: Mimi siamini kuwepo
kwa MwenyeziMungu mpaka nimuone kwa urefu na mapana. (Astaghafiru llah).
Sheikh:- Jee wewe unampenda
mumeo?
Bibi :-
ndiyo.
Sheikh
:- Mimi sisadiki.
Bibi :- Kwa nini?
Sheikh:- Siamini kama
unampenda mumeo mpaka niyaone hayo mapenzi kwa marefu na mapana na uzito na
rangi yake.
Bibi :- Mapenzi yapo lakini
haiwezekani kuyaona kama yalivyo.
Sheikh :- Basi MwenyeziMungu
ni mfano ulio bora zaidi, sisi tunaamini kuwa yupo ingawaje hatuna uwezo wa
kumjua jinsi alivyo. Na vingapi tunaviamini ingawaje havionekani. Usingizi
unatujia na sisi hatuujuwi jinsi ulivyo na wala hatujuwi vipi na wapi
unatokea. Kuamka pia, furaha na hata kuna wengi ambao hawaelewi umeme ukoje
lakini wanaamini kuwepo kwake na kuna mambo mengi ya aina hiyo.
Kwa dalili za kiakili na za
kunukuu tunaelewa kwamba MwenyeziMungu ni tofauti na viumbe Vyake, na kwa
ajili hiyo sifa zake lazima zitofautiane na sifa za viumbe vyake, kwa sababu
kila kiumbe kina upungufu wa sifa, lakini yeye Subhanahu Wa taala ndiye
aliyekamilika.
Kutoka Kwake tumejulishwa
Wasfu Wake pamoja na ubainifu, kwa hivyo tuziamini na kufuata kama
alivyotujulisha katika kitabu chake kitukufu pamoja na Mafundisho ya Mtume
wake (SAW) bila kuuliza juu ya mfano Wake.
MwenyeziMungu anasema:-
"Hakuna chochote mfano Wake Naye ni
Mwenye kusikia na Mwenye kuona."
(Al -Shuraa -11)
Kwa hivyo Yeye ni Mwenye
Kusikia na Mweye Kuona lakini kuona na kusikia kwake si kama kuona na kusikia
kwa viumbe vyake na sisi hatuna ilimu ya kumzunguka na kumjua
vilivyo na Yeye ndiye Aliye Mkuu Aliye Juu.
MwenyeziMungu amemuumba
binaadmu akiwa na akili, ili aweze kutambua uhakika wa mambo, na kwa akili
hiyo aweze kupambanua baina ya haki na batili na aweze kuelewa kinachomdhuru
na chenye manufaa naye. Ndiyo sababu aliyepoteza akili akawa amenyanyuliwa
kalamu (haandikiwi dhambi wala thawabu). Mwenyezi Mungu akaipa akili hiyo
uwezo wa aina nyingi.
MwenyeziMungu amempa
binaadamu uwezo wa kufikiria juu ya mambo mbali mbali ili uwezo huo umsaidie
katika kupanga mambo yake na kuyafikiria.
Lakini uwezo huo (wa kufikiria) una udhaifu na pia una mipaka yake.
Mfano; ukisifiwa ju ya mji,
utaanza kufikiria mambo mengi juu ya mji huo, lakini unapokuja kuuona mji huo
utaona kwamba sio kama vile ulivyokuwa ukiufikiria.
Mfano mwingine; Mlango
ukigongwa utajua kwamba yupo mtu anayegonga mlango, lakini uwezo wako wa
kufikiria unashindwa kumjua ni nani anayegonga mlango huo, urefu wake, upana
wake, rangi yake nk.
Kwa hivyo Nguvu za Akili
zimevuka mpaka wa mlango na kuweza kujuwa kuwa yupo anayegonga, lakini Uwezo
wa Kufikiria umeshindwa kuupenya mlango na kumjua mgongaji.
(MwenyeziMungu Ndiye Mwenye
Sifa Tukufu) Akili inaamini kuwa yupo Mwenyezi Mungu, lakini Uwezo wa
Kufikiria unashindwa kufikiria jinsi MwenyeziMungu alivyo.
"Hakuna chochote mfano Wake
Naye ni Mwenye Kusikia na Mwenye Kuona".
As Shuura- 11
MwenyeziMungu ana majina
mazuri mazuri tisini na tisa, atakayeyahifadhi (na kutimiza wajibu wa majina
hayo) ataingia Peponi. Na Mtume (SAW) ametujulisha juu ya majina mengine mbali
ya hayo.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na MwenyeziMungu ana majina
mazuri mzuri muombeni kwayo."
(Al -Aaraf -180).
Miongoni mwa majinaa Yake
mazuri ni haya yafuatayo:-
Al Waahid - Mmoja
Aliyepekee.
Al Ahad - Mmoja.
Assamad - Anayetegemewa Kwa
Kila Mahitaji Naye Hana Shida Ya Kitu
Al Qayyum - Anayesimamia
Kila Jambo.
Al Khaliq - Muumbaji.
Al Musawwir - Mfanyaji Wa
Sura Za Kila Aina Ya Viumbe
Al Rahman - Mwenye
Kuneemesha Neema Kubwa Kubwa
Al Rahim - Mwenye Kuneemesha
Neemesha Ndogo Ndogo.
Al Latif - Mpole
Al Razzaq - Mtoaji Wa
Riziki.
Al Waasi-a
- Ambaye Rehema Na Elimu
Yake Imeenea Kila Mahali
Al Adhiym - Aliye Mkuu
Al Aziz - Mshindi
Asiyedhalilika
Al Hakiym - Mwenye Hikima
Al Aliym - Ajuwaye Kila Kitu
Al Haafidh - Mwenye
Kuhifadhi (Kulinda).
Al Haadi - Mwenye Kuongoza.
Al Muhu-yi - Mwenye
Kuhuyisha
Al Mumiyt - Mwenye Kufisha
Al Waarith - Atayebaki Baada
Ya Kutoweka Viumbe Vyote
Dalili Zilizo Wazi Juu Ya Ukweli Wa Utume Wa Muhammad (SAW)
MwenyeziMungu huwapa Mitume
wake ushahidi (Miujiza) wa kuthibtisha ukweli wa ujumbe wao ili wasikanushwe
na watu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Kwa hakika tuliwapeleka
Mitume wetu kwa dalili waziwazi (Miujiza)".
Al Hadiyd -25
Na MwenyeziMungu amempa
Mtume Muhammad (SAW) ushahidi ulio wazi kabisa pamoja na dalili zisizo na
shaka ambazo ni Miujiza, ikiwemo ifuatayo:
MwenyeziMungu ameijaalia
miujiza ya Muhammad(SAW) iwe ya daima ili iwe ni hoja kwa watu wote hadi siku
ya kiama na akaijaalia Qurani tukufu kuwa ni muujiza wenye nguvu kupita zote,
na akaihifadhi isiweze kubadilishwa (maneno yake).
MwenyeziMungu anasema:-
"Basi jee mtu aliye na dalili wazi itokayo kwa Mola
wake (naye ni Nabii Muhammad) na anaifuata (dalili hiyo) shahidi atokaye kwake
MwenyeziMungu (Nayo ni Quran) na kabla yake kilikuwa kitabu cha Musa
kilichokuwa kiongozi na rehema (nayo ni Taurat ambayo ilitaja habari za Nabii
Muhammad)(anaweza kuwa muongo? Hawezi kuwa muongo), basi hao (walioongoka)
wanamuamini yeye, na atakayemkataa katika makundi (ya maadui) basi moto ndio
mahali pa miadi yao".
(Hud -17)
Ushahidi huu wa Qurani upo
wa aina nyingi zinazothibitisha miujiza yake, na tutazitaja baadhi yake.
Maandishi ya Qurani
yanatokana na herufi za 'hija-a' (alfabeti), (Alif, Be, Te, Thee …….)
Na maneno ya wanaadamu
yatokana na herufi hizi hizi, lakini ufasaha wa Qurani
umewafanya wanadamu na majini washindwe kuleta sura ndogo za mfano wa
Qurani.
Unaposikia hotuba
iliyotolewa kwa ufasaha au nyimbo nzuri, zinakupendeza, lakini ukishasikiliza
mara nyingi, hamu yake inaondoka, hii ni kwa sababu maneno yanayosemwa na
wanadamu kwa kawaida huchosha kuyasikia yanapokaririwa mara kwa mara.
Lakini Waislamu mara ngapi
na ngapi wanaisoma SuratulFatiha au Sura ndogo ndogo za Qurani, au mara ngapi
wanahitimisha Msahafu na kurudia tena na tena bila kuchoka wala kutokwa na
hamu. Hii ina maana gani? Bila shaka hii ni dalili iliyo wazi kwa kila mwenye
akili kwamba Qurani ni maneno ya MwenyeziMungu yasiyochosha (juu ya kukaririwa
kwake).
Na Qurani imewabishia
wanaoukanusha ukweli wake, walete sura moja yenye mfano wake.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na mkiwa mna shaka kwa hayo
tuliyomteremshia Mtumwa wetu basi leteni sura moja (iliyofanywa na mtu) mfano
wake na muwaite waungu wenu wasiokuwa MweyeziMungu (wakusaidieni) ikiwa
mnasema kweli. Na msipofanya, na hakika hamtafanya kamwe, basi uogopeni moto
ambao kuni zake ni watu na mawe, uliowekewa makafiri."
(Al - Baqrah -23-24)
Hapana aijuwae ghaibu
isipokuwa MwenyeziMungu, na Qurani imeeleza habari nyingi za ghaibu. Na hii ni
dalili kwamba Qurani imetoka kwa MwenyeziMungu na kwamba Muhammad (SAW)
aliyekuja nayo ni Mtume wa MwenyeziMungu.
1) Zifuatazo ni miongoni mwa
habari za ghaibu zilizoelezwa katika Qurani tukufu:-
Wakati Wafursi (Iran) waliokuwa wakiabudu moto (na masanamu)
walipowashinda Warumi waliokuwa watu wa Kitabu, katika nchi ya Palastina,
washirikina wa Makka (waliokuwa wakiabudu masanamu kama wao) walifurahi sana
na wakawa wanawaambia Waislamu (kwa kuwatisha), kwamba mwisho wao utakuwa kama
mwisho wa Warumi.
Habari hizi ziliwahuzunisha sana
Waislamu (ambao pia ni watu wa kitabu, Qurani). Ndipo MwenyeziMungu
alipoteremsha aya isemayo:-
"Aliyf Laam Mym.
Warumi wameshindwa katika
nchi iliyo karibu na (na nchi ya bara Arabu nayo ni Shamu), nao baada ya
kushindwa kwao watashinda.
Katika miaka michache. Amri
hii ni ya MwenyeziMungu kabla (yake) na baada (yake) na siku hiyo Waislamu
watafurahi.
Kwa nusura ya MwenyeziMungu.
Humnusuru Amtakaye Naye ni Mwenye Nguvu na Mwenye Rehema.
(Hii ni) ahadi ya MwenyeziMungu,
MwenyeziMungu havunji ahadi Yake lakini watu wengi hawajui."
(Al Rum - 1-6).
Zilipoteremshwa aya hizi
Waislamu wakawa wanazisoma mara kwa mara wakiwadhihaki washirikina kwa vile
walivyowatabiria kwamba na wao Waislamu watashindwa kama walivyoshindwa
Warumi.
Mmoja katika makafiri
akashindana na Abubakar (RA) kwa mali (dau), akidai kwamba Wafursi hawatoweza
kushindwa kwa muda huo mchache. "(BIDHI-I-SINIYN)", neno lililotumika katika
aya hiyo maana yake ni baina ya
miaka mitatu na tisa, sio zaidi, na Abubakar(RA) alikubali kushindana na
kafiri huyo kwa dau, na hii ilikuwa kabla haikuharamishwa kushindana kwa mali
(dau), na Mtume (SAW) aliruhusu ushindani huo.
Makafiri wakasimama pamoja
na kafiri mwenzao aliyeingia katika ushindani, na Waislamu wakawa wanaingoja
ahadi iliyotolewa na MwenyeziMungu itimie, na Mtume(SAW) akasema kuwa
(BIDHI_I) ni baina ya tatu na tisa.
Unabii (wa Mtume(SAW))
uliingizwa katika mtihani mkubwa, kwa sababu umekuja na habari kutoka kwa
MwenyeziMungu zikibashiri ushindi wa Warumi ambao hivi karibuni tu walishindwa
vibaya sana, na hapakuwa na dalili kuwa wangeweza kushinda tena. isitoshe
waadi uliowekwa (kuwa watashinda) ulikuwa chini ya miaka kumi. Na habari hizo
zimeelezewa kwa njia ya kuwafahamisha watu kuwa Warumi watashinda bila shaka
yoyote ile;
"Ahadi Ya Mwenyezi Mungu
Ambae Havunji Ahadi Yake Lakini Watu Wengi Hawajui".
Na Makafiri wote wanaelewa
kwamba Muhammad (SAW) ni mwenye akili timamu kupita wote, na kwamba
asingejiingiza katika mtihani kama huu angekuwa hana uhakika utokao kwa Mola
wake pamoja na Imani aliyo nayo juu ya Mola wake.
Haikupita miaka saba na
ahadi ya MwenyeziMungu ikatimia. Wafursi walishindwa, Waislamu wakafurahi, na
ukweli wa Mtume(SAW) ukadhihiri, na watu wengi wakaamini na kuingia katika
dini ya MwenyeziMungu.
2) Majaribio mengi yalifanywa na Washirikina wa Makka pamoja na Mayahudi
ya kutaka kumuuwa Mtume(SAW), kivita, na kwa kufanya hila mbali mbali. Juu ya
hayo, MwenyeziMungu akateremsha aya katika Qurani zikimhakikishia Mtume wake
(SAW) kwamba maadui wake hawawezi kumdhuru.
Mwenyezi Mungu anasema;
"Na kumbuka tulipokwambia
'Hakika Mola wako amekwisha wazunguka hao watu (wabaya)"
(Al - Israa -60).
Na akasema:-
"Ewe Mtume!
Fikisha uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako na kama hutofanya basi
hukufikisha ujumbe wake na MwenyeziMungu atakulinda na watu."
(Al -Maidah -67)
Baada ya kuteremka aya hizi,
Mtume (SAW) akawaamrisha Masahaba waliokuwa wakimlinda (RA) kwa kuwaambia;
"Enyi watu! towekeni
msinilinde tena, maana MwenyeziMungu Aliyetukuka keshatoa waadi wa kunilinda
na hakuna awezaye kunidhuru".
Ibnu Jarir, Al Tirmidhy na
Al Hakim.
Ingawaje mbinu nyingi
zilifanywa za kutaka kumuuwa
Mtume(SAW), lakini MwenyeziMungu alizishinda kama alivyoahidi.
Baada ya kufa kwa
Mtume(SAW), watatu miongoni mwa Makhalifa wanne Waongofu (Al Rashidiyn, nao
ni, Omar Othman na Ali (R.Anhum)), wote waliuliwa, ingawaje wakati huo Uislamu
ulikuwa na nguvu zaidi na ukafiri ulikuwa umekwisha toweka na amani ilikuwa
imeenea kwa ajili ya usalama wa Makhalifa hao, na wakati Mtume(SAW) hapakuwepo
na amani kama hiyo, lakini Ulinzi Wake MwenyeziMungu ndio uliomwokoa Mtume
(SAW) aliyekuwa na uhakika juu ya ahadi hiyo na akaendelea kuwalingania watu,
akawaondoa walinzi wake na MwenyeziMungu akamtimizia yale Aliyomuahidi.
3) Mitume (Alayhimu
Ssalaam), hapo mwanzo walikuwa wakiteremshwa mmoja baada ya mwengine, lakini
baada ya kuja kwa Mtume (SAW), hakuteremsha Mtume mwengine,
na hii inasadikisha kauli ya MwenyeziMungu isemayo:-
"Muhammad si baba wa yeyote
katika wanaume wenu bali yeye ni Mtume wa MwenyeziMungu na mwisho wa Mitume.
Na MwenyeziMungu ni Mjuzi wa kila kitu."
Haa Miym Sajdah -53
(Fusilat)
Hii ni ahadi inayozungumzia
Ghaybu iliyosadikishwa na karne nyingi zilizokuja baada ya Mtume Muhammad
(SAW) ikisadikisha kuwa hapana Mtume baada ya "Mwisho wa Mitume" (Muhammad
(SAW)).
Mwenyezi Mungu anasema;
"Tutawaonyesha (ukweli wa)
maneno yetu haya katika nchi za mbali na katika nafsi zao wenyewe mpaka
IWABAINIKIE kwamba haya ni kweli. Je! Haikutoshi kwa Mola wako kuwa Yeye ni
mjuzi wa kila kitu?"
Ha Miym Sajdah - 53
(Fusilat)
Ahadi ya Mola wetu imetimia
katika wakati wetu huu. Makafiri ambao bado HAUKUWABAINIKIA ukweli wa dalili
za Mwenyezi Mungu, wakaziona dalili za MweyeziMungu katika kuumba kwake,
katika sehemu mbali mbali za dunia. Hawakuweza kuyaona hayo isipokuwa kwa
kutumia vyombo na njia za kisasa kabisa, mfano wa ndege, manowari zinazozama
baharini (Submarine), vyombo ambavyo hapo zamani wanadamu hawakuwa
wakivimiliki.
Ikawabainikia kwamba
MwenyeziMungu ndiye aliyempa Muhammad(SAW) siri hizo katika kuumba (akaweza
kuzijua tokea miaka elfu moja mia nne aliyopita), wakati hapakuwa na vyombo
vya kufanyia uchunguzi wa kielimu (maabara) na pia hapakuwa na ndege wala
manowari zinzozama baharini na hii
ikawa ni namna nyingine ya miujiza ya
Qurani ikiwabainishia makafiri ukweli wa ujumbe aliokuja nao Mtume
Muhammad (SAW) na ukweli wa dini
hii.
Miongoni mwa miujiza hiyo ni
:-
1) Hapana aliyekuwa akijua
kwamba asili ya sayari zote pamoja na nyota zake ni moshi, mpaka zana za
uchunguzi wa sayansi zilipoendelea sana na wachunguzi kuona mabaki ya moshi
katika hali ya kubadilika zikigeuka kuwa nyota hadi wakati wetu huu.
Na MwenyeziMungu anasema :-
"Kisha akazielekea mbingu na
zilikuwa moshi basi akaziambia mbingu na ardhi. "Njooni mkipenda msipende".
Vyote viwili vikasema; 'Tumekuja hali ya kuwa wenye utiifu".
Haa mym Sajdah- 11.
2) Wachunguzi hivi karibuni
tu wamegundua kuwa nyota bado zinaendelea kuumbwa na kwamba mikusanyiko ya
nyota (Galaxies) inazidi kubaidika kila moja mbali na nyingine na kwa njia hii
ikajulikana kuwa nyota zilizo angani zingali zinatawanyika na kuwasaika na
kuenea mbali zaidi.
MwenyeziMungu amesema:-
"Na mbingu tumezifanya kwa
kudra yetu na hakika sisi ndio wenye uwezo wa kuzieneza".
(Al - Dhariyyat -47).
3) Wachunguzi hivi karibuni
pia wamegundua kwamba hapo mwanzoni mwezi ulikuwa ukiwaka na kutoa mwangaza
wenyewe bila ya kumulikiwa na jua na hatimaye mwangaza huo ukafutika na kwamba
mwangaza tunaoupata kutoka mwezini wakati wa usiku asili yake ni mwangaza wa
jua unapoumulika mwezi kisha mwangaza huo unaturudia sisi.
MwenyeziMungu anasema:-
"Kisha tumeifuta
(tumeuondosha mwangaza) ishara ya usiku na tukaifanya ishara ya mchana yenye
mwangaza."
Bani -Israil - 12
(Israa).
Maulamaa wa tafsiri wamesema
(Ishara ya usiku ni mwezi na Ishara ya mchana ni jua) na Ibni Abbas (RA)
amesema;
"Mwezi ulikuwa ukitoa
mwangaza kama jua".
Maulamaa wa tafsiri
wamesema;
"Maana ya kauli yake
MwenyeziMungu;
"Tumeifuta ishara ya usiku"
ni
(Tumeufuta mwangaza wake).
Kisha Qurani ikataja juu ya
mwezi na taa yake (jua )
MwenyeziMungu anasema:-
"Ni mwenye kuleta baraka
yule aliyezijaalia nyota mbinguni na akajaalia humo taa (jua ) na mwezi
unaonga'ra".
(Al -Firqan -61).
Zingatia! MwenyeziMungu
amesema "(TAA)" (Siraajan), na lau kama mwezi unatoa mwangaza kama jua (ambalo
lenyewe linawaka na kutowa mwangaza), basi MwenyeziMungu angalisema "TAA
MBILI" (Siraajayni) na asingelisema "TAA moja"(Siraajan).
4)
Watu, hapo zamani walikuwa wakidhani kwamba anayepaa kueleka anga za
juu huvuta pumzi kwa raha zaidi, lakini
baada ya mwanadamu kuunda ndege za kisasa na kuruka angani akagundua
kwamba anayepaa juu, kifua chake hudhikika
na kufikia hali ya juu ya
kudhikika na hii ni kwa sababu
hewa hupungua kila anapopaa na kuelekea juu zaidi.
MwenyeziMungu anasema:-
"Basi yule ambaye
MwenyeziMungu anayemtaka kumuongoza hukifungulia kifua chake Uislamu; na yule
ambaye MwenyeziMungu anataka kumhukumu kupotea hufanya kifua chake kizito
kinaona taabu kubwa (kufuata huo Uislamu) kama kwamba anapanda mbinguni
(kusikokuwa na pumzi) ".
(Al - An -am -125)
5) Hakuna aliyekuwa
akifikiria kwamba jabali limezama ndani ya ardhi kama vigingi mpaka wataalamu
walipogundua kwamba chini ya ardhi hii ngumu tunayoishi juu yake, pana tabaka
laini mfano wa tope zito na kwamba kila jabali lina (mfano wa) mizizi sehemu
ya chini inayopiga mbizi ndani ya
tabaka hizo laini na kuizuia ardhi ngumu hii tunayoishi juu yake isije ikazama
katika ardhi laini iliyo chini yetu .
MwenyeziMungu amesema:-
"Na milima kuwa kama vigingi
vya ardhi ".
(A n
-Nabaa -7)
"Na tukaweka katika ardhi
milima (yenye kuthibiti barabara katika ardhi) ili isiwayumbishe".
(Al _Anbiyaa -31).
6) Wataalamu wakagundua pia
kwamba maji yanapoteremka ndipo mmea unapoota na kwamba mmea hutoa mada yenye
rangi ya kijani yenye kutengeneza punje na matunda. Na kutokana na mada hii ya
kijani matunda na punje za nafaka hupatikana.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na yeye ndiye aliyeteremsha
maji kutoka mawinguni, na kwayo tunaotesha mimea ya kila kitu. Kisha
tunapeleka kuchipua (majani ya) kijani (mada ya kijani 'chlorophyl'). Katika
(mimea) hiyo tukatoa ndani yake punje zilizopangana."
(Al _Anam -99)
1)
Wachunguzi pia wamegundua kwamba mimea yote ipo dume
na jike, na haya hayakuwa yakijulikana hapo mwanzoni.
MwenyeziMungu anasema:-
"Ametukuka MwenyeziMungu
alieumba dume na jike katika (vitu) vyote. Katika vile vioteshayo ardhi na
katika nafsi zao (wanaadamu) na katika vile wasivyovijua."
(Yaasin -36)
8) Madaktari wamegundua kwamba mishipa ya hisia (nerves) inayohisi
maumivu ya kuungua na inayohisi ukali wa baridi ipo penye ngozi tu, kama
ilivyo mishipa mengine ya hisia. (yote imo penye ngozi). Na hii ndio sababu
inayomfanya mtu ahisi maumivu ya sindano anayopigwa na daktari pale inapoingia
ngozini, ama sindano ikishazama ndani ya mwili (katika nyama) maumivu
hutoweka.
Na Qurani imebainisha kwamba
maumivu ya kuungua hupatikana penye ngozi tu. MwenyeziMungu anasema:-
"Hakika wale waliozikataa
aya zetu tutawaingiza katika moto. Kila ngozi zao zitakapowiva tutawabadilisha
ngozi nyengine badala ya zile ili wawe wanaonja uchungu wa adhabu (maisha).
Hakika MwenyeziMungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hekima.
(An -Nisaa -56).
9) Wataalamu pia wakagundua kwamba maziwa ya wanyama hukamilika
utengenezaji wake baada ya kupita baina ya mavi ndani ya utumbo mdogo wa
mnyama huyo (small intestine), na vibakiavyo humo hutoka vikiwa mfano wa
kinyesi. Wakati hapo mwanzoni mabaki hayo yalikuwa mfano wa choo maji maji.
(mfano wa matapishi). Baada ya kupita katikati ya mavi yaliyo ndani ya utumbo
mdogo, maziwa hupitia katika damu (ili yasafike kutokana na uchafu wa
kinyesi), na yanapotoka katika damu husafishwa maziwa hayo kutokana na damu
katika matiti.
MwenyeziMungu anasema:-
"Na bila ya shaka katika
wanyama mna mazingatio makubwa kwa ajili yenu. Tunakunywisheni katika vile
vilivyomo matumboni mwao (vikitoka) baina ya choo na damu (nayo ni maziwa
tukakunywisheni), maziwa safi mazuri kwa wanywao".
(Al - Nahli -66).
10) Hapana aliyekuwa akijua
kwamba chini ya bahari kuna mawimbi ya ndani mbali ya mawimbi ya juu
tuyaonayo, na watu hawakuwa wakijuwa kwamba sehemu za chini ya bahari (kubwa)
ni giza (totoro). MwenyeziMungu amewaumba samaki wanaoishi sehemu za chini ya
bahari kubwa wakiwa na (mfano wa) taa ili iwaangazie njia katika viza hivyo.
Na hapana aliyekuwa akijua
kwamba mawimbi, kwa sababu ya kutotulia kwake huirudisha juu miale ya mwangaza
na kusababisha miale hiyo isifike chini ya bahari, na kwa hivyo hupatikana
giza lnalozidi kila uendapo chini ya bahari mfano wa mawingu yanapozuwia
mwangaza wa jua kufika juu ya ardhi.
Siri zote hizi MwenyeziMungu
amezieleza katika aya moja tu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Au (amali zao zile mbaya)
ni kama giza katika bahari yenye maji mengi inayofunikwa na mawimbi na juu
yake kuna mawimbi na juu yake (kuna) mawingu. Giza hili juu ya hili, (hata)
anapoutoa mkono wake anakaribia asiuone (kwa kiza kilivyoshtadi ) na ambaye
MwenyeziMungu hakumjaalia nuru hawi na nuru."
(An - Nur -40)
Siri hizi na nyenginezo
zilizomo katika anga za juu, chini ya bahari, chini ya ardhi, ndani ya matumbo
ya wanyama, ndani ya miti na jinsi binaadamu alivyoumbika, binaadamu hawakuwa
wakizijua isipokuwa katika zama hizi za karibu na baada ya kuunda vyombo na
ala za kisasa zilizomwezesha kuzijua siri hizi.
Basi ni nani aliyemjulisha
Muhammad(SAW) siri hizi miaka elfu na mia nne iliyopita wakati ambapo siku
hizo hapakuwa na ndege wala submarine wala hapakuwa na uvumbuzi wa kisayansi?
Haya yote yanamthibitishia
kila mwenye akili akiwa yupo Amerika au Urusi. Bara hindi au Uchina, Ulaya au
Australia kwamba Qurani hii imeteremshwa kwa ujuzi wa MwenyeziMungu.
MwenyeziMungu anasema:-
"Sema'; Ameteremsha haya
yule ajuaye siri za mbinguni na ardhini."
Al Furqan - 6
Huu pia ni ushahidi kwa kila
mwenye akili kwamba Muhammad(SAW) ni Mtume wa MwenyeziMungu.